• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

KIGOMA YAENDELEA KUTEKELEZA KWA MAFANIKIO ZOEZI LA UTOAJI HUDUMA YA MSAADA WA KISHERIA KWA WANANCHI

Posted on: January 4th, 2023

Kazi nzuri zinazotekelezwa katika utoaji Msaada wa kisheria Mkoani Kigoma zimeendelea kuzaa matunda na kupunguza machungu katika jamii kutokana na uwepo wa changamoto ya uelewa duni kuhusu masuala ya kisheria hali inayosababisha upotevu wa mali, muda, uwepo wa chuki na uvunjifu wa amani na badala yake kuimarisha upatikanaji wa haki kwa wahitaji wa msaada huo.

Msaada wa kisheria ni huduma inayojumuisha utoaji wa ushauri wa kisheria, usaidizi na uwakilishi wa watu wasiokuwa na uwezo kumudu gharama za uendeshaji wa kesi  katika ngazi mbalimbali za kimahakama nchini.

Sheria inayoongoza utoaji wa Huduma ya Msaada wa Kisheria Na. 1 ya Mwaka 2017, imelenga kuwafikia wananchi walioko katika Mazingira yanayofikika na yale yasiyofikika isipokuwa kwa Kibali maalum ili kutoa msaada, ushauri, uwakilishi kwa watu hao kutokana na kukosa uwezo wa kumudu gharama za uendeshaji wa kesi au uelewa mzuri kuhusu haki zao kisheria.

Serikali katika Mkoa wa Kigoma imeendelea kutekeleza zoezi hilo kwa ufanisi na mafanikio makubwa pamoja na uwepo wa uhaba wa vitendea kazi na watendaji, huku ikama ikibainisha uwepo wa wasaidizi wa kisheria 117, watoa huduma ya msaada wa kisheria 10 na mawakili 12 ambao wanafanya kazi kwa ukaribu na kuendelea kuwajengea uwezo wasaidizi wa kisheria.

Msajili Msaidizi wa watoa Huduma za Msaada wa Kisheria Ngazi ya Mkoa Msafiri Nzunuri, anasema awali changamoto ya uelewa wa Masuala ya kisheria kwa wananchi ilikuwa kubwa, hali iliyosababisha mrundikano wa kesi Mahakamani na ongezeko la malalamiko kuhusu masuala ya upatikanaji wa Haki katika Jamii.

Anaeleza kuwa, kupitia mazoezi mbalimbali ya hamasa, uelimishaji pamoja na uhabarishaji kwa Umma kwa kutumia vyombo vya Habari na mitandao ya kijamii, wameweza kuwafikia wananchi na kuwajengea uwezo na uelewa kuhusu huduma za msaada wakisheria.

Anabainisha kuwa, idadi ya waliopata Msaada huo  kwa kipindi cha Julai 2020 hadi Juni 2021 huduma za kisheria zilitolewa zilifanikiwa kuwafikia watu 526, huku rufaa zikiwa 81 na kesi zilizofanikiwa kufikishwa mahakamani zikiwa 15.

Msafiri anabainisha kuwa, kwa kipindi cha Julai 2021 hadi Juni 2022, idadi ya waliopata msaada wa kisheria kimkoa ni watu 917 ambapo kati yao ni Wanaume 136 na Wanawake 777 ikiwa ni ongezeko la watu 251.

Aidha anaongeza kuwa katika kipindi cha Julai 2021 hadi 2022, Msaada wa kisheria umefanikiwa kuwagusa  watoto 913 ambapo kati yao wakiume wakiwa 136 na wakike 777 na kuhakikisha watoto hao haki zao zimepatikana kisheria.

‘‘Watoto wamekuwa waathirika wakubwa wa kutosimamiwa ipasavyo kwa Sheria katia jamii na inapaswa kulichukulia suala hili kwa uzito vinginevyo tutajenga Taifa lenye watu wenye chuki na visasi kutokana na maumivu waliyowahi kuyapitia’’anasema Nzunuri.

Nzunuli anabainisha kuwa, changamoto zinazokwamisha kufikiwa kwa ufanisi ni utendaji usiozingatia kanuni wa Mabaraza ya Ardhi ya Kata, hususani katika kutafuta suluhu za migogoro ya Ardhi katika maeneo mbalimbali ya vijiji.

Anafafanua kuwa, baadhi ya watendaji katika Mabaraza hayo, wamekuwa wakijipa majukumu ya kuhukumu badala ya kutoa suluhu hali inayoendelea kusababisha wananchi kutoridhika na maamuzi yanayotolewa na kuamua kujielekeza katika ngazi mbalimbali za kimahakama ili  kutafuta ufumbuzi wa kisheria wa masuala yao.

Anasema uelewa mdogo wa Jamii kuhusu Sheria unaendelea kusababisha changamoto kubwa katika utekelezaji wa mipango kazi iliyowekwa na Serikali ili kutekeleza jukumu hilo lenye dhamira ya kutoa haki kwa wanaoshindwa kuipata kutokana na sababu za kiuchumi na uelewa wa kisheria.

Ili kukabiliana na changamoto hizo Nzunuri anasema, wameendelea kushirikiana na  wadau mbalimbali wa masuala ya kisheria katika kuwajengea uelewa wananchi  kwa kuendesha mafunzo mbalimbali pamoja na kutoa Elimu kwa mabaraza ya kata mkoani hapa.

‘‘Vyombo vya Habari pamoja na wadau kutoka Taasisi zisizo za kiserikali za HEKA, KIPAFO, WAPAO, BUPAO, MAPAO, KIPACE, BAKAIDS, KIVULINI, TWCC, KIVIDEA, WPC, KIWODE, KIWOHEDE, TGNP na WLAC wameendelea kuwa msaada katika kutoa elimu na kufanikisha utekelezaji wa kazi mbalimbali zinazohusu utoaji wa Misaada ya kisheria kwa jamii katika Mkoa’’anasema.

Katika kuhakikisha huduma za kisheria zinaendelea kutolewa katika wigo mpana na utoshelevu, Nzunuri anasisitiza kuwa Serikali kwa kushirikiana na wadau wa Sheria wataendelea kuhakikisha utoaji bora wa huduma kwa kuwajengea uwezo wasaidizi wa Sheria katika Halmashauri zote, kuendeleza ushirikiano wa karibu na mawakili, kuongeza idadi ya  walengwa pamoja na kuzidi kutoa Elimu kwa Jamii.

Huduma za kisheria zimeendelea kuwa msaada mkubwa mkoani Kigoma na Tanzania kwa ujumla kutokana na kuwafikia wahitaji katika maeneo fikika na yasiyofikika ila kwa kibali Maalum ambako mahitaji ni makubwa.

Aidha, Huduma za Msaada wa kisheria zimekuwa zikiwanufaisha kwa kiasi kikubwa wanawake, wazee, watoto na watu wenye mahitaji maalum ambapo baadhi ya wanajamii wasioheshimu sheria , haki za binaadamu, utu na mahusiano mema wamekuwa wakidhulumu kwa makusudi au kwa kutokuelewa haki za Raia za kisheria za makundi hayo.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • RC ANDENGENYE AKABIDHI VITENGO VITENGO VYA LISHE MKOA NA WILAYA UVINZA

    May 09, 2025
  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa