• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

KIGOMA YAENDELEA KUIMARISHA MIKAKATI KUKABILIANA NA VIFO VYA MAMA WAJAWAZITO NA WATOTO

Posted on: December 19th, 2022

Idara ya Afya Mkoa wa Kigoma imejipanga kuendelea kuchukua hatua mbalimbali ili  kukabiliana na changamoto za vifo vya wanawake wajawazito, watoto wachanga pamoja na kufuatilia visababishi vya vifo hivyo.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Dkt. Jesca Lebba, amesema kwa kipindi cha Januari hadi Oktoba 2022 hali ya vifo vya wanawake vitokanavyo na uzazi mkoani hapa ikiwa ni wanawake 85 pamoja na watoto wachanga 632.

Amezitaja baadhi ya sababu za vifo hivyo kuwa ni kifafa cha Mimba, Shinikizo la Damu, kuharibika kwa mimba, Marelia kali, wajawazito kutokamilisha matibabu, kutohudhuria kliniki kwa mfululizo pamoja na umbali kutoka kwenye Makazi hadi maeneo ya kutolea huduma za Afya.

‘‘Changamoto ya uhaba wa magari ya kusafirisha wagonjwa, baadhi ya maeneo kutofikika kwa urahisi nyakati za Masika, pamoja na uelewa mdogo wa jamii kuhusu tahadhari za kiafya kwa Mama wajawazito zimeendelea kusababisha ongezeko la vifo hivyo mkoani hapa’’ alisema.

Baadhi ya hatua zinazoendelea kuchukuliwa na Idara ya Afya Mkoani Kigoma katika kukabiliana na vifo vya wanawake na watoto ni pamoja na kuongeza huduma za vituo vya upasuaji na uzazi, kutoa mafunzo kwa watoa huduma za uzazi, kuimarisha mfumo wa usafirishaji wagonjwa, kuimarisha huduma ya kliniki mkoba pamoja na kuongeza watumishi wa kujitolea na mikataba.

Amezitaja hatua nyingine kuwa ni pamoja na kufanya zoezi la kufuufuatiliaji wa kina na kuendelea kufanya utafiti ili kubaini sababu za vifo vinavyotokea katika Jamii  na vituo vya kutolea huduma, hususani vinavyowahusu wanawake na watoto na kuchukua hatua stahiki.

‘’Tunaendelea kufanya zoezi la ukusanyaji wa Damu salama,  kuanzisha vitengo vya huduma za Dharura kwa watoto wachanga na kuelimisha jamii kuhusu tahadhari mbalimbali kwa ajili ya usalama wa Mama wajawazito na watoto wachanga’’alisema Lebba.

Baadhi wa wakina mama wamekiri kuwepo kwa changamoto ya ukosefu wa Elimu ya Afya kwa jamii katika kutoa msaada kwa mama wajawazito hususani wanapokuwa katika hali ya ujauzito hadi wakati wa kujifungua.

‘‘Kumekuwa na Ushirikiano hafifu katika jamii hususani nyakati za kujifungua, jamii inatakiwa kubadilika ili kuongeza ushrikiano hali itakayonusuru changamoto mbalimbali zinazowakabili mama wajawazito na kusababisha vifo hivyo’’ Amesema Debora Mwampeta.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • RC ANDENGENYE AKABIDHI VITENGO VITENGO VYA LISHE MKOA NA WILAYA UVINZA

    May 09, 2025
  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa