• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

KIGOMA INAMAZINGIRA RAFIKI YA UWEKEZAJI-RUGWA

Posted on: August 27th, 2024


Katibu Tawala Mkoa wa Kigoma Mhe. Hassan Rugwa amesema Mkoa wa Kigoma ni miongoni mwa mikoa yenye mazingira rafiki kiuwekezaji nchini kutokana na hali yake kijiografia, kuendelea kuimarika kwa miundombinu ya uchukuzi na kutolea huduma za jamii pamoja na kupakana na nchi jirani za Burundi, Congo DR na Zambia.

Mhe. Rugwa ametoa kauli hiyo alipozungumza wakati akifungua semina ya uhamasishaji wa uwekezaji wa ndani mkoa wa Kigoma iliyolenga kujadilina kubainisha fursa  zilizopo mkoani hapa, iliyoratibiwa na Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC) kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma na kufanyika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma.

Amesema serikali ya awamu ya Sita imewekeza zaidi ya Shilingi Tril.12 mkoani Kigoma kwa ajili ya kuchechemua uchumi wa Mkoa na wananchi kwa ujumla kupitia fursa zilizopo kupitia uboreshaji mkubwa wa miundombinu  ya kutolea huduma za jamii, uchukuzi na usafirishaji pamoja na kuimarisha masoko ya kimkakati.

Rugwa amesema amezitaja fursa hizo kuwa zipo katika sekta ya Kilimo, Uvuvi, biashara, mifugo sambamba na uwekezaji kupitia viwanda mbalimbali.

Amewaeleza washiriki wa semina hiyo kuwa, uhitaji wa nchi ya Congo DR katika kusafirisha mizigo hufikia Kontena 5000 huku hali halisi ya uwezo wa nchi ni kusafirisha chini ya Kontena 1400 kwa mwaka.

Aidha amesema kiwango halisi cha uhitaji wa abiria kusafiri baina ya Tanzania na Congo ni watu 8000 huku uwezo uliopo ni kusafirisha abiria 3000 kwa Mwaka.

‘’Nitumie nafasi hii kuwahimiza kuzitazama fursa hizo ili wafanyabiashara muweze kuwekeza katika maeneo hayo kutokana na serikali kuandaa mazingira wezeshi kwa ajili ya kufanimisha uwekezaji wenu’’ amesema Rugwa.

Amesema barabara zinazouunganisha mkoa na mikoa jirani zimeshakamilika kwa kiasi kikubwa huku usafiri wa anga ukiendelea kuimarika kufuatia serikali kufanya upanuzi wa uwanja wa ndege wa Kigoma kutoka Km 2 hadi kufikia Km.3.5 ili kuruhusu ndenge za kimataifa kutua mkoani Kigoma.

Upande wa Ardhi, Mhe Rugwa amesema sambamba na mkoa kuwa na maeneo mengi ya wazi yanayoruhusu kufanya uwekezaji ikiwemo ujenzi wa viwanda au kuanzisha Kilimo cha  mazao ya kimkakati, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa imetenga kiasi cha hekta 140 kwa ajili ya uwekezaji katika eneo maalum la uwekezaji la mkoa (Kigoma Special Economic Zone-KiSEZ)

‘’ Niwahimize wafanyabiashara kuwekeza katika kilimo cha zao la chikichi ili kukabiliana na uhaba wa mafuta ya kupikia ndani na nje ya mkoa sambamba na kuwekeza kwenye ardhi kama walivyofanya wawekezaji katika kiwanda cha Sukari Kasulu’’amesema.

‘’Upande wa Afya, Serikali inajenga Hospitali ya Kanda sambamba na Tawi la Chuo Kikuu cha Muhimbili ambacho kitakuwa na wanafunzi kati ya 3000 hadi 10,000, idadi hiyo ya wanachuo ni kubwa sana hivyo itatoa fursa ya kiuchumi kwa wenye nyumba za kupangisha pamoja na wafanyabiashara ndogondogo’’ amesema Rugwa.

Amesema sambamba na hayo serikali iko kwenye hatua za mwisho kuunganisha mkoa na gridi ya Taifa ili kutatua changamoto ya muda mrefu ya kutotosheleza kwa umeme mkoani Kigoma.

Upande wake mshiriki wa Semina hiyo ambaye pia ni mfanyabiashara mkoani hapa Mousen Abdallah ameishauri serikali kupitia kikao hicho kukutana na wafanyabishara wa nchi jirani ya Congo DR  ili waweze kujadili na kuondoa changamoto mbalimbali za kibishara.

Aidha ameiomba serikali kuandaa mafunzo ya pamoja baina ya wafanyabiashara wa Kigoma yatakayolenga kuwajengea uwezo  katika kutambua majukumu ya Kituo cha uwekezaji cha Taifa jambo litakalowapa fursa ya kutambua namna bora ya kukopa na kuendesha mitaji yao kwa kuzingatia kanuni mbalimbali za kwa faida.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa