• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

Kigoma Mwenyeji wa Maonesho ya SIDO Kitaifa 2021

Posted on: January 20th, 2021

Maonesho ya Kitaifa ya Shirika la Viwanda Vidogo SIDO yanatarajiwa kufanyika Mkoani Kigoma mwezi septemab 2021 katika Halmashauri ya Kasulu.

Akiongea na waandishi wa habari Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mhe. Thobias Andengenye amesema SIDO imeweka utaratibu wa kufanya maonesho ya kitaifa kila mwaka, ambapo tayari maonesho ya kwanza yalifanyika mkoani Simiyu, ya pili yalifanyika mkoani Singida na ya tatu yamepangwa kufanyika Wilayani Kasulu mkoani Kigoma kwa siku 10 kuanzia tarehe 21 hadi 30 Sptemba, 2021.

Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma itashirikiana bega kwa bega na SIDO kufanikisha maonesho hayo. Inatarajiwa wajasiriamali wapatao 700 wakiwemo kutoka nchi za jirani Burundi, Kenya, Rwanda, Uganda na kwingieko wanaotengeneza bidhaa mbalimbali za uhandisi, usindikaji vyakula, nguo, bidhaa mchanganyiko watahudhuria. Aidha Taasisi mbalimbali za Serikali na zisizo za kiserikali zipatazo 40 zinazotoa huduma zitahudhuria maonesho hayo.

Muhimu ni kuwa SIDO Mikoa yote ya Tanzania bara watahudhuria wakileta teknolojia/ mashine mbalimbali zinazorahisisha uchakataji wa mazao na vitu mbalimbali.

“Nitoe wito kwa Halmashauri zote na Taasisi zote za Serikali na zisizo za Kiserikali, Miradi ya maendeleo, Makampuni makubwa na madogo yaliyopo mkoani Kigoma kushiriki ipasavyo katika maandalizi ya maonesho haya. Pia natoa hamasa kwa wajasiriamali na wananchi wote kushiriki katika maonesho kwa kuwa yatalenga kufungua fursa katika mkoa wa Kigoma” amesema Mkuu wa Mkoa.

Ametaja kuwa maonesho hayo yanalenga mambo mambo mbalimbali ikiwemo kutangaza shughuli na huduma za SIDO pamoja na wadau mbalimbali kwa wananchi ili wanufaike nazo, Kuhamasisha ubora wa bidhaa, kupanua soko na kutangaza bidhaa za wazalishaji wadogo wa ndani, kuona na kuonesha teknolojia mbalimbali ambazo ni zetu, rahisi, muafaka na rafiki wa mazingira

Ameongeza kuwa waoneshaji watapata fursa ya kuuza bidhaa zao na kujenga mahusiano na umoja wa kibiashara miongoni mwa wazalishaji, wafanyabiashara, wakulima na taasisi mbalimbali pia kuwawezesha wenyeviwanda vidogo kujifunza miongoni mwao na hatimaye kuzalisha bidhaa bora na zinazohimili ushindani na kukubalika katika soko.

Aidha katika maonesho hayo yatawawezesha wajasiriamali wazalishaji wadogo kubadilishana uzoefu na ujuzi wa kiufundi na kibiashara na kuwaunganisha wajasiriamali wadogo na wakubwa ili waweze kushikiana kibiashara na hatimaye kuwepo kwa sura nzuri ya uzalishaji mali nchini.

Amewaomba na kuwasisitiza wananchi kujipanga kupokea ugeni na kuchangamkia fursa mbalimbali zitakazopatikana ili Mkoa wetu wa Kigoma uzidi kusonga mbele kimaendeleo.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa