• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

KAMBI MAALUM YA MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA YAZINDULIWA MKOANI KIGOMA

Posted on: May 6th, 2024

MKUU WA WILAYA YA KIGOMA SALUM KALLI AKIZUNGUMZA NA WAKAZI WA MKOA WA KIGOMA SAMBAMBA NA MADAKTARI BINGWA NA WATENDAJI WENGINE WA IDARA YA AFYA WALIOHUDHURIA KWENYE UZINDUZI WA  KAMBI YA MATIBABU YA MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN MKOANI KIGOMA.

Na. Gladness Kusaga-Kigoma.

Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Salum Kalli ametoa wito kwa wakazi ndani wa ndani na nje ya Mkoa wa Kigoma wenye changamoto za kiafya kuhudhuria Kambi maalum ya Madaktari Bingwa wa Dkt. Samia Suluhu Hassan inayolenga kutoa  huduma za kibingwa za kimatibabu iliyozinduliwa katika Hospitali ya Mkoa ya Maweni Kigoma leo Mei 6, 2024.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Kalli amesema Serikali kupitia madaktari hao bingwa wa magonjwa mbalimbali, imejipanga kuwafikia wagonjwa wote watakaohudhuria katika kambi hiyo na kuwapatia matibabu.

Amefafafanua kuwa, Hospitali ya Rufaa Maweni Kigoma kupitia Idara ya Afya Mkoa, imepokea madaktari bingwa sitini (60) kutoka Kanda mbalimbali ambao watakuwa tayari kutoa huduma kwa wagonjwa watakaojitokeza hadi katika muda wa ziada ili kuhakikisha wote wanaguswa na huduma hiyo.

Kalli ameishukuru Ofisi ya Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kigoma kwa kushirikiana na Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa Maweni kwa kuwaalika madaktari bingwa kwa ajili ya kutatua changamoto mbalimbali za kiafya kwa wakazi wa mkoa wa Kigoma na maeneo jirani.

Naye Mwakilishi wa Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Dkt. Albert Paschal amesema mkoa umekuwa na changamoto ya muda mrefu ya kupata huduma za kibingwa kwa ukaribu hivyo wananchi wanapaswa kuitumia fursa hiyo ili kuepuka gharama ya kufuata huduma hizo katika mikoa mingine.

Ametoa wito kwa Wataalam wa Afya watakaoshiriki zoezi hilo kuzingatia miiko ya utoaji wa huduma ya Afya na Taaluma ya matibabu sambamba na kuviomba vyombo vya Habari kushiriki katika kusaidia kutoa taarifa kwa jamii ili wananchi wafahamu kuhusu uwepo wa kambi hiyo.

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa ya Maweni Kigoma, Dkt. Stanley Binagi amesema katika kipindi cha Siku tano za Kambi hiyo zitatolewa huduma bobezi za matibabu ya Pua, Koo, uchunguzi wa Saratani ya mlango wa kizazi na matiti  na changamoto za ugonjwa wa Moyo.

Amezitaja huduma nyingine kuwa ni upasuaji kwa ajili ya matibabu ya mifupa, matibabu ya kibingwa ya Moyo, uzazi kwa kina mama na kina baba, matibabu ya kibingwa ya moyo kwa watoto waliozaliwa na tatizo hilo, ngozi, figo pamoja na maradhi mengine ya ndani.

Aidha kupitia Kambi hiyo, Dkt. Binagi amesema wenye changamoto za macho na kuhitaji miwani watapatiwa bure, kufanyika kwa uchunguzi na matibabu ya magonjwa ya akili sambamba na msongo wa mawazo.

Kambi hiyo ya Siku tano ya matibabu ya madaktari bingwa itakuwepo kuanzia leo Mei 6, 2024 ikihusisha madaktari kutoka Hospitali ya Mkoa wa Kigoma Maweni, Hospitali ya Kitete ya Tabora, Katavi na Sumbawanga.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa