• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

JAMII YATAKIWA KUZINGATIA MLO KAMILI KUEPUKA UDUMAVU

Posted on: July 10th, 2023

Tabia ya Ulaji usiozingatia makundi Maalum ya Vyakula yenye virutubisho muhimu kwa Afya umetajwa  kuchangia kuendeleza uwepo kwa hali ya utapiamlo, uzito pungufu, ukondefu na udumavu kwa watoto mkoani Kigoma.

Kauli hiyo imetolewa na Katibu Tawala Mkoa wa Kigoma Mhe. Albert Msovela alipozungumza kwenye Kikao Jumuishi cha Lishe Ngazi ya Mkoa kwa kipindi cha Januari hadi Machi 2023 kilichofanyika mkoani hapa.

Amesema Mkoa unazalisha vyakula lishe vya kutosha lakini bado kumekuwepo na changamoto ya utapiamlo mkali pamoja na udumavu unaoathiri watoto na wanawake wajawazito, kutokana na jamii kushindwa kuzingatia ulaji unaohusisha makundi muhimu ya vyakula.

‘’Nitoe Wito kwa wataalam wa Afya, kuongeza nguvu katika kutoa  Elimu ya Lishe kupitia majukwaa mbalimbali ili wananchi waweze kutambua umuhimu wa mlo kamili kwa lengo la kusaidia kukabiliana na hali  ya utapiamlo na udumavu mkoani hapa’’ amesisitiza Msovela.

Msovela amewaelekeza Timu ya Uendeshaji wa Huduma za Afya Mkoa kufanyia kazi Taarifa na takwimu za hali ya Afya na upatikanaji wa chakula zinazotolewa na watendaji ngazi za wilaya ili kubaini uweli wa Taarifa hizo na kuzifanyia kazi kuendana na uhakisia wake.

Ameitaka Timu hiyo kuendelea kukutana na wadau wanaotekeleza Afua mbalimbali za Afya mkoani Kigoma kwa kila robo Mwaka na kuweka wazi mikakati yao pamoja na hatua wanazochukua katika  utekelezaji wa Afua hizo.

Pia Msovela ameielekeza Idara ya Elimu Msingi na Sekondari kuhakikisha utaratibu wa wanafunzi kupata Chakula shuleni unatekelezwa kwa asilimia mia moja pamoja na kuwataka kufuatilia na kufahamu hali ya ubora wa chakula kinacholiwa na wanafunzi katika shule za Sekondari za Bweni zilizopo mkoani hapa.

Naye Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Dkt. Jesca Leba amesema Idara ya Afya kupitia wataalam wa Lishe wameendelea kutoa Elimu ya utambuzi, uandaaji, utunzaji na ulaji wa makundi mbalimbali ya chakula ili kudumisha utamaduni wa kula mlo kamili.

Amesema iwapo walaji watatambua na kuzingatia  muhimu wa kula vyakula kuendana na makundi yenye virutubisho Muhimu, Jamii itaachana na tabia ya kula vyakula kutokana na urahisi katika upatikanaji wake bali kwa kuzingatia mahitaji muhimu ya kiafya mwilini.

Akiwasilisha Taarifa ya Utekelezaji wa Afua za Lishe, Afisa Lishe Mkoa James Ngalaba amesema hali ya udumavu kimkoa kwa Mwaka 2022 ilikuwa ni watoto 119,864 sawa na asilimia 27.1, udumavu uliokithiri watoto 38,480 sawa na Asilimia 8.7, uzito pungufu 53,961 sawa na Asilimia 12.2,  pamoja na ukondefu ikiwa ni watoto 11,057.6 sawa na Asilimia 2.5.

Akitaja mikakati wa kukabiliana na kupunguza changamoto za lishe, Afisa Lishe Mkoa amesema  wameendelea kuchukua hatua mbalimbali ikiwemo  kufanya usimamizi shirikishi wa mara kwa mara  katika vituo vya kutolea huduma za Afya, kujenga uelewa kuhusu masuala ya lishe kwa watendaji pamoja na wahudumu wa Afya ngazi ya Jamii na katia vituo vya kutolea huduma za Afya vya Serikali.

Ameendelea kuitaja mikakati hiyo kuwa ni pamoja na kushirikisha wadau mbalimbali wa Afua za Lishe pamoja na kuimarisha mifumo ya utoaji elimu hiyo katika vituo vya kutolea huduma za Afya.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • RC ANDENGENYE AZINDUA RASMI ZOEZI LA UGAWAJI VYANDARUA KIMKOA

    May 27, 2025
  • JAMII INAPASWA KUZINGATIA CHANJO KUJILINDA NA MARADHI

    May 20, 2025
  • MRADI WA UHIFADHI MAZINGIRA WAZINDULIWA KIGOMA

    May 15, 2025
  • RC ANDENGENYE AKABIDHI VITENGO VITENGO VYA LISHE MKOA NA WILAYA UVINZA

    May 09, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa