• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

JAMII YATAKIWA KUZINGATIA KANUNI ZA USAFI WAKATI WOTE

Posted on: December 30th, 2022

Jamii mkoani hapa imetakiwa kuzingatia kanuni za usafi wakati wote  ili kuepuka uwezekano wa kuibuka kwa magonjwa ya mlipuko.

Rai hiyo imetolewa na Mhasibu Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Johson Gamba alipokuwa akichangia mada kwenye Kikao cha Kamati Jumuishi ya Lishe Mkoa kwa Kipindi cha Julai-Septemba 2022, kilichofanyika katika Ukumbi wa Katibu Tawala Mkoani hapa.

Amesema jamii imejenga tabia ya  kuzingatia masuala ya usafi na kuchukua tahadhari mbalimbali yanapotokea magonjwa ya mlipuko na kisha athari za maradhi hayo zinapopungua hujisahau na kuzirejea tabia za awali, jambo linaloruhusu kuendelea kujirudia kwa maradhi hayo.

‘‘Katika maeneo mengi ya Taasisi za Serikali na zile Binafsi pamoja na yale yenye mikusanyika mikubwa ya watu, tahadhari za uwepo wa vitakasa mikono zimeanza kupuuzwa, aidha maeneo mengi ya mijini changamoto ya udhibiti na uhifadhi wa taka imeendelea kushuhudiwa, hali inayohatarisha usalama wetu kwa ujumla’’ amesema Gamba.

Dkt. Jesca Lebba ambaye ni Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, amesema Mkoa unaendelea kukabiliana na changamoto za kiafya ikiwemo suala la  udumavu kwa kuendelea kutekeleza Afua mbalimbali za Lishe ikiwa ni pamoja na kuwaagiza wazabuni wanaolisha katika shule mbalimbali mkoani hapa kusaga mahindi kwa ajili ya chakula cha wanafunzi hao katika mashine zenye utaratibu wa kuongeza virutubishi.

Ameeleza kuwa, wameendelea kuhamasihsa kilimo cha viazi lishe katika shule za Msingi za Sekondari zenye maeneo yanayoruhusu kilimo cha zao hilo ili kuhakikisha wanafunzi wanakula chakula hicho na kujenga tabia ya kilimo cha zao hilo lenye manufaa makubwa kiafya.

Akiwasilisha Taarifa ya Utekelezaji wa Mkataba wa Lishe kwa kipindi cha Julai-Septemba 2022, Bi. Naomi Rumenyela amesema kuwa, utekelezaji wa Afua za lishe umefanyika kwa ufanyaji kazi za maadhimisho ya Siku ya Afya na Lishe, ukaguzi usalama wa chakula, upimaji wa chumvi, unasishi kwa wahudumu wa Afya ngazi ya Jamii,  kufuatilia zoezi la utoaji wa Fedha za kuratibu upatikanaji Lishe Shuleni na utioaji wa madini ya Foliki kwa wajawazito.

Aidha amesema shughuli za utoaji wa matone  nyongeza ya Vitamini A, ulishaji wa watoto katika vituo vya kutolea huduma na kufanya maadhimisho ya ulishaji wa chakula shuleni yalifanyika kwa ukamilifu katika kipindi kilichopangwa.


Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • RC ANDENGENYE AZINDUA RASMI ZOEZI LA UGAWAJI VYANDARUA KIMKOA

    May 27, 2025
  • JAMII INAPASWA KUZINGATIA CHANJO KUJILINDA NA MARADHI

    May 20, 2025
  • MRADI WA UHIFADHI MAZINGIRA WAZINDULIWA KIGOMA

    May 15, 2025
  • RC ANDENGENYE AKABIDHI VITENGO VITENGO VYA LISHE MKOA NA WILAYA UVINZA

    May 09, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa