• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

JAMII YATAKIWA KUKABILIANA NA UTAPIAMLO ILI KULINDA AFYA YA MTOTO

Posted on: November 20th, 2023

Wakazi mkoani Kigoma wameaswa kuzingatia ulaji unaojumuisha makundi mbalimbali ya vyakula ili kukabiliana na janga la utapiamlo na kujenga msingi wa Afya bora kwa watoto.

Wito huo umetolewa na Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Kigoma Nesphoty Sungu alipofungua kikao cha Kamati ya Lishe mkoa kwa kipindi cha Julai hadi Septemba 2023, na kusisitiza kuwa pamoja na mkoa kuzalisha chakula cha kutosha bado kunachangamoto ya uwepo wa utapiamlo.

Amesema maeneo mengi ya mkoa yanazalisha aina mbalimbali za vyakula lakini changamoto kubwa inatokana na wakazi kujenga mazoea ya kutokula vyakula kwa kuzingatia mlo kamili hivyo kusababisha kuendelea kuwepo uwepo wa changamoto utapiamlo na udumavu.

Amesema  Idara ya Afya Mkoa kupitia Kitengo cha Lishe imefanikiwa  kupambana na kupunguza udumavu kutoka watoto 300,000 hadi 119,000 ikiwa ni sawa na kutoka Asilimia 43. Hadi kufikia 27.

Ameendelea kufafanua kuwa sambamba na suala la lishe Jamii inapaswa kusimamia suala la makuzi ya watoto ikiwemo  kuwapa ulinzi dhidi ya vitisho na unyanyasaji  ili kuwafanya waweze kuishi salama pamoja na kuwajengea ujasiri wa kuweza kukabiiana na changamoto mbalimbali katika mazingira yao.

Aidha Sungu ameisisitiza jamii kuendelea kukabiliana na janga la utapiamlo kwani husababisha madhara makubwa kwa watoto chini ya miaka mitano ikiwemo vifo, ulemavu wa kudumu pamoja na athari mbalimbali zitokanazo na maradhi yasiyotibika na kuiletea jamii mzigo mkubwa.

Akiwasilisha Taarifa ya utendaji kazi kwa Kipindi cha Julai hadi Septemba 2023, Mratibu wa Lishe Mkoa wa Kigoma James Ngaraba amesema katika kuhamasisha suala la lishe, mkoa unaratibu na kusimamia utaratibu wa kila kijiji kuadhimisha Siku ya lishe kila baada ya miezi mitatu.

Amesema kwa kipindi cha Aprili hadi Juni 2023 kiwango cha Shule zinazotoa chakula shuleni kimkoa kimefikia Asilimia 65.7, viwanda vinavyoongeza virutubishi kwenye chakula ikipanda kutoka Asilimia 37.5 hadi 51.1, huku ulaji wa chakula shuleni ukipanda kutoka Asilimia 65.7 hadi 68.2.

Ameendelea kufafanua kuwa katika kipindi hicho, idadi ya watoto waliogundulika na ukondefu imeshuka kutoka Asilimia 0.5 hadi kufikia 0.3, kilibatumbo kutoka Asilimia 0.3 hadi 0.1 na utapiamlo mkali kutoka Asilimia 0.5 hadi 0.4.

Afisa Afya Hospitali ya Mkoa wa Kigoma ya Maweni Francisca Lutumula amesema changamoto inayoikabili jamii ni kushindwa kuelewa dalili na Athari za utapiamlo hali inayosababisha madhara makubwa kwa watoto.

‘’Tunaendelea kutoa elimu kwa jamii ili waweze kufahamu dalili na madhara yatokano ya upungufu wa lishe kwani baadhi wananchi huhusisha madhara hayo na Imani za kishirikina jambo linaloweza kuwaathiri watoto kwa kiasi kikubwa’’ amesema Francisca.

Wakichangia agenda mbalimbali zilizowasilishwa kupitia kikao hicho, wajumbe wameshauri Kitengo cha Lishe Mkoa kufuatilia, kubaini na kudhibiti uzalishaji na usambazaji wa chumvi isiyo na madini joto.

Wamesisitiza watendaji wa kitengo hicho kuendelea kufuatilia na kuwabaini wazalishaji kisha kuwapa miongozo itakayowataka kuzingatia kuingiza sokoni chumvi itakayowekewa madini hayo muhimu kwa usalama wa Afya za walaji.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa