• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

JAMII YAONYWA KUMALIZA VITENDO VYA UKATILI NJE YA MAHAKAMA

Posted on: March 8th, 2024

MKUU WA MKOA WA KIGOMA THOBIAS ANDENGENYE AKIWASALIMIA WANANCHI WALIOJITOKEZA KUSHIRIKI KILELE CHA MAADHIMISHO YA SIKU YA WANAWAKR DUNIANI KILICHOFANYIKA KIMKOA KATIKA KATA YA MAKERE WILAYANI KASULU.

MKUU WA WILAYA YA KASULU ISSACK MWAKISU(KULIA) PAMOJA MA AFISA MAENDELEO YA JAMIIMKOA WA KIGOMA MSAFIRI NZUNURI WAKIFUATILIA JAMBO WALIPOSHIRIKI KILELE CHA MAADHIMISHO YA SIKU YA MWANAMKE KIMKOA.

Jamii mkoani Kigoma imetakiwa kuachana na tabia ya kumaliza mashauri       yanayohusu vitendo vya ukatili wa kijinsia nje ya taratibu za kisheria na kusababisha usugu wa vitendo hivyo.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye alipozungumza kwenye kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake duniani ambayo kimkoa yamefanyika wilayani Kasulu na kusisitiza kuwa asilimi kubwa ya matukio hayo hufanywa katika ngazi ya familia.

‘’Tafiti zinaonesha Asilimia Sitini ya matukio ya unyanyasaji na ukatili wa kijinsi hufanywa na watu wa karibu au ndani ya familia huku kukiwa hakuna hatua za kisheria zinazochukuliwa hali inayosababisha matukio hayo kujirudia mara kwa mara na kuleta athari ya muda mrefu miongoni mwa wanajamii’’ amesema Mkuu huyo wa Mkoa.

Katika kufikia kasi ya mabadiliko ya kisiasa, kiuchumi na kijamii kwa kundi hilo mkoani Kigoma, mkuu huyo wa mkoa amewaelekeza wakurugenzi wa halmashauri  kuimarisha uratibu na usimamizi wa shughuli za kielimu na hamasa kuhusu uwekezaji na masuala ya kijinsia katika maeneo yao kwa lengo la kuleta ustawi wa jamii.

Mkuu wa Mkoa amewaelekeza watendaji hao wa Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo kuendelea kutekeleza mpango kazi wa Taifa wa kutokomeza vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto, huku akiitaka jamii kutumia nafasi zao kutofumbia macho vitendo hivyo kwani athari kubwa kwa watendewa.

Andengenye amewakumbusha  wanawake mkoani hapa kutumia fursa za maboresho makubwa ya miundombinu ya uchukuzi sambamba na  nishati ya Umeme ili kujiimarisha kiuchumi na kujiletea maendeleo wao wenyewe, jamii zao na Taifa kwa ujumla.

‘‘Niendelelee kuwasihi wakazi katika maeneo yote ambayo miundombinu mipya imejengwa au kufanyiwa maboresho, tuendelee kuitunza ili itusaidie kwa muda mrefu kwani kutokufanya hivyo tutajikuta tunarejea kwenye adha zilizotukabili siku zilizopita’’  amesisitiza Mkuu huyo wa mkoa.

Katika kuimarisha mfumo wa Utawala bora, Mkuu wa mkoa amewakumbusha wanawake mkoani hapa, wajibu wao katika kugombea nafasi mbalimbali za uongozi ili waweze kupata fursa ya kuonesha umahiri wao katika Ngazi mbalimbali za kiutawala.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • RC ANDENGENYE AKABIDHI VITENGO VITENGO VYA LISHE MKOA NA WILAYA UVINZA

    May 09, 2025
  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa