• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

JAMII MKOANI KIGOMA YATAKIWA KUZINGATIA AFUA ZA LISHE ILI KUKABILIANA NA UDUMAVU

Posted on: September 30th, 2022

BAADHI YA MADIWANI, VIONGOZI WA SERIKALI NA WATUMISHI WA MANISPAA YA KIGOMA-UJIJI WAKIWA WAMEJIANDAA KUUPOKEA MWENGE WA UHURU KATIKA  UWANJA WA SHULE YA SEKONDARI BURONGE, LEO TAREHE 30/SEPTEMBA 2022.

Jamii mkoani Kigoma imetakiwa kuzingatia Afua za Lishe katika kukabiliana na tatizo la udumavu kwa wakina mama na watoto ili Taifa liweze kuendelea kuwa na kizazi chenye afya bora.

Akikagua Huduma za Lishe kabla ya kuweka jiwe la Msingi katika Kituo cha Afya Buronge kilichopo  Halmashauri ya Manispaa  Kigoma-Ujiji Mkoani hapa, Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Mwaka 2022 Sahili Geraruma aliwataka wakazi kuyapa kipaumbele masuala ya Lishe  ili kuimarisha Afya ya Mama, mtoto na Jamii kwa ujumla.

‘‘Suala la umuhimu wa Afya tunapaswa kulipa kipaumbele kwani bila kuwa na Afya bora hatutoweza kufanya kazi na kuuimarisha uchumi wetu binafsi na Taifa kwa ujumla’’alisema Geraruma.

Sambamba na ukaguzi huo, Kiongozi huyo wa Mbio za Mwenge kitaifa, alipata fursa ya kukutana, kuzungumza kisha kutoa  chakula chenye thamani ya zaidi ya Shilingi Milioni Nne Fedha kutoka Halamshauri, kwa Konga la Halmashauri ya Manispaa  Kigoma-Ujiji.

‘‘Kuishi na Virusi vya Ukimwi sio tatizo bali tatizo ni kutokuwa mfuasi sahihi wa dawa za kufubaza makali ya virusi hivyo’’alisisitiza Geraruma.

Naye Mtaalam wa Masuala ya Lishe Dafroza Bernard, alisema makuzi ya akili na mwili wa mtoto  hutegemea zaidi mlo kamili na wenye ubora.

‘‘Mkoa wa Kigoma ni miongoni mwa mikoa yenye tatizo la udumavu na kwa kiasi kikubwa linachangiwa  na  baadhi ya wakazi kutokubali kuipokea elimu ya Afua za lishe na kuamua kubadilika ili  kuzingatia Afua hizo’’

‘‘Nakiri kuwepo kwa changamoto za kiuchumi lakini hata wanaomudu kupata vyakula vya kutosha hawazingatii utaratibu wa kula mlo kamili’’ alisema Dafroza.

Upande wake Mwenyekiti wa Konga la  Halmahsauri Manispaa Kigoma-Ujiji, Athumani Rajabu alisema wameguswa na tukio hilo la kutolewa kwa chakula huku akisisitiza jamii iendelee kufanya matendo yanayogusa utu kuliko  unyanyapaa kwa wanaoishi na maambukizi ya virusi vya UKIMWI.

Alisema tabia ya unyanyapaa imeendelea kujitokeza kwa baadhi ya watu wasio na Elimu kuhusu ugonjwa wa UKIMWI huku akiishukuru serikali kwa kuendelea kutoa elimu pamoja na Dawa za kufubaza maradhi hayo.

‘‘Kwa sasa hatuna usumbufu wa kufuatilia dawa mara kwa mara kwani ukiwa mfuasi mzuri unaweza kupewa dawa za kutumia kwa kipindi cha miezi mitatu hadi sita kutegemeana na hali ya utoshelevu wa viini kinga mwailini’’ alisema  Rajabu.

Mbio hizo za Mwnge wa Uhuru kwa Mwaka 2022 katika Halmashauri ya Manizpaa ya Kigoma-Ujiji, zimezindua, kutembelea, kuweka jiwe la msingi na kutoa chakula  ambapo huduma na miradi hiyo ikiwa na Thamani ya  zaidi ya Shilingi Bilioni 1.6

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa