• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

JAMII YAASWA KUTUMIA MASANDUKU YA MAONI KUBAINISHA CHANGAMOTO ZAO

Posted on: November 21st, 2022

Jamii mkoani hapa imetakiwa kutumia fursa ya uwepo wa masanduku ya maoni yanayopatikana kwenye vituo vya Serikali vinavyotoa huduma za kijamii kwa lengo la kupaza sauti na kubainisha changamoto mbalimbali zilizopo katika maeneo wanayoishi ili ziweze kupatiwa ufumbuzi.

Rai hiyo imetolewa na Mshauri wa Mradi wa Uimarishaji wa Mifumo katika Sekta za Umma Kanda ya Magharibi, Samwel Mashindika wakati wa kikao kazi kilicholenga kuwajengea uwezo baadhi ya wakuu wa Idara na vitengo vinavyohusika na utekelezaji wa Mradi huo katika kufuatilia Taarifa za utendaji kazi kilichofanyika Halmashauri ya wilaya ya Uvinza.

Amesema masanduku hayo yanatoa Uhuru kwa wananchi kufikisha Taarifa za kero na changamoto za utoaji na upatikanaji huduma katika taasisi za kiserikali na hatua mbalimbali zimeendelea kuchukuliwa na kuleta matokeo chanya baada ya kupatikana kwa utatuzi wa changamoto hizo.

‘’Baadhi ya wananchi wamekua waoga kufika ofisini na kuwaambia wahusika moja kwa moja kuhusu changamoto zinazojitokeza katika utendaji kazi wao kwa kuhofia kuibuka kwa uhasama baina yao na wanaolalamikiwa, bali kupitia mfumo wa masanduku ya maoni, ujumbe huwafikia walengwa na maamuzi kufanyika bila kuathiri mahusiano ya pande zote mbili’’ amesema.

Mratibu wa Mradi huo wa Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3 Plus) Kanda ya Magharibi Bi. Rose Mwangilima, amesema Masanduku hayo yameendelea kuleta matokeo chanya kwa kung’amua kero mbalimbali zinazoikabili jamii ikiwemo kutopatikana kwa huduma kwa ukamilifu, ukiukwaji wa haki za binaadamu na mapungufu katika utekelezaji wa masuala mbalimbali ya kisheria.

Amesema Malalamiko mengi yanayotolewa na kushughulikiwa yamekuwa yakijitokeza katika Nyanja za Elimu, Afya, Utawala, Sheria pamoja na Usalama wa Raia.

‘‘Maoni hutolewa na wananchi kuendana na mahitaji yanayowagusa kama jamii na iwapo wahusika watayafanyia kazi na walengwa kukubali kuwajibika ama kuwajibishwa, kero nyingi za wananchi zitabainika, kufanyiwa kazi na kuondoa sintofahamu zinazojitokeza katika jamii’’ amesema Bi. Mwangilima.

Upande wake Afisa TEHAMA Mkoa wa Kigoma Bi. Ashura Sadick, ameshauri Taasisi zote za Serikali zihakikishe zinakuwa na Sanduku la Maoni pamoja Kamati hai zitakazohakikisha malalamiko yanapokelewa na kushughulikiwa kwa wakati. Aidha amesisitiza kuwa, watakaohusika na usimamizi wa masanduku hayo wawe huru kutekeleza wajibu wao bila kuingiliwa katika utendaji kazi.

PICHA: Wataalam wa Idara na vitengo mbalimbali kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Halmashauri ya wilaya Uvinza pamoja na waratibu wa Mradi  wa Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3 Plus) Kanda ya Magharibi wakiwa katika Majadiliano wakati wa Kikao kazi  kilichofanyika katika  halmashauri ya Uvinza, kikiwa na Lengo la kuwajengea uwezo baadhi ya wakuu wa Idara na vitengo vinavyohusika na utekelezaji wa Mradi huo katika kufuatilia Taarifa za utendaji kazi kwa ngazi mbalimbali Serikalini.


Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa