• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

JAMII MKOANI KIGOMA YATAKIWA KUENDELEA KUTUNZA MAZINGIRA

Posted on: June 5th, 2023

Jamii mkoani hapa imetakiwa kuchukua hatua za Makusudi katika kuhakikisha Mazingira yanakuwa salama  kwa  kuepuka kutupa taka ovyo na kuteketeza kwa usahihi zile zilizopo ili kudumisha Sera na mikakati endelevu ya kukabiliana na uharibifu wa Mazingira.

Kauli hiyo imetolewa na Mratibu wa  Mazingira Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Bi. Mercy Mbungulu alipoongoza zoezi la Usafi wa Mazingira katika Eneo la Uwanja wa Ndege wa Mkoa wa Kigoma kisha kutoa Elimu ya utunzaji wa Mazingira  udhibiti wa taka ngumu, kwa baadhi ya wadau wa Mazingira ikiwa ni katika kuadhimisha kilele cha Siku ya Mazingira Duniani.

Amesema katika wiki ya Maadhimisho hayo, wamejikita katika kutoa Elimu na kushiriki kufanya usafi wa Mazingira kwenye Maeneo yanayotoa huduma muhimu za kijaii yanayohusisha muingiliano mkubwa wa watu kutoka katika maeneo mbalimbali ya ndani na nje ya Mkoa.

‘’Leo tumeshiriki kufanya Usafi katika Eneo la Uwanja wa Ndege wa Mkoa wa Kigoma kwa sababu eneo hili ni kati ya Maeneo yanayoingiza wageni wengi mkoani Kigoma wakitokea ndani na nje ya nchi, hivyo tumefanya hivi ili kutoa hamasa na Elimu kwa watumishi wa eneo hili pamoja na wakazi wa Maeneo ya jirani na uwanja huu’’ amesema Mbungulu.

Amesisitiza kuwa ’’Tumetoa Elimu kuhusu udhibiti wa Mifuko ya Plastiki kwa vijana wa vyuo, katika maeneo ya Stendi, vituo vya Afya, Masoko pamoja na maeneo mengine ya kutolea huduma za kijamii ili kuongeza uelewa kuhusu madhara na umuhimu wa udhibiti wa bidhaa hizo zinazochangia uzalishaji wa taka ngumu’’

Mbunguru  amefafanua kuwa, kilele cha Maadhimisho hayo ni muendelezo wa juhudi za Serikali mkoani Kigoma katika kufikisha Elimu na kuhamasisha suala la utunzaji wa Mazingira katika Jamii.

Naye Meneja wa Baraza la Taifa la uhifadhi wa Mazingira Kanda ya Magharibi  Mkoa wa Kigoma Edgar Mgira, amesema moja wapo ya Jukumu wanalotekeleza kupitia Siku hiyo ni kutoa Elimu ya Usafi  wa Mazingira kwa watumishi wa Uwanja wa ndege mkoa wa Kigoma pamoja na wadau wengine wa Mazingira kwa lengo la kupunguza Madhara yatokanayo na utupaji wa Taka ngumu ikiwemo mifuko ya Plastiki.

Ameongeza kuwa mpango mkakati uliopo ili kuimarisha na kujenga uelewa kwa wakazi mkoani hapa kuhusiana na usafi wa Mazingira ni pamoja na kutembelea wadau mbalimbali wa Mazingira katika maeneo yao pamoja na kutumia vyombo vya Habari kutoa Elimu na miongozo ya kudhibiti uchafuzi wa Mazingira.

Baadhi ya wadau wa Mazingira mkoani hapa walioshiriki zoezi hilo, wameiomba Serikali kupitia Mamlaka zinazosimamia uhifadhi na usimamizi endelevu wa Mazingira mkoani hapa, kulifanya suala la usafi kuwa endelevu badala ya kusubiri nyakati za Maadhimisho.

wamesema Suala la kuhamasisha usafi, kusimamia na hata kuwawajibisha wasiofuata taratibu zilizowekwa na Serikali linatakiwa kufanyika nyakati zote ili kudhibiti tabia Hatarishi kwa usalama wa Mazingira kwa ajili ya Maisha ya kizazi cha sasa na kijacho.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa