• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

JAMII KIGOMA YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUMALIZA MIGOGORO NJE YA MAHAKAMA

Posted on: February 1st, 2023

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Kigoma  Mhe. Lameck Mlacha ameiasa Jamii kujenga tabia ya kutatua migogoro yao na kuimaliza kwa njia ya usuluhishi nje ya mifumo ya Mahakama ili kuepuka upotevu wa fedha pamoja na muda ili kutumia rasilimali hizo katika kujiletea maendeleo.

Jaji Mlacha ametoa Rai hiyo alipozungumza kwenye hafla fupi ya Maadhimisho ya Kilele cha wiki na Siku ya Sheria  ambayo kimkoa yamefanyika kwenye viwanja vya Mahakama Kuu Kanda ya Kigoma na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali ngazi ya Mkoa na wilaya, Vyama vya Siasa, Dini, watumishi wa Idara ya Mahakama pamoja na wadau mbalimbali wa Sheria mkoani Kigoma.

‘‘Jamii iwe tayari kumaliza migogoro nje ya vyombo vya Sheria kwa sababu Fedha na Muda vinapotea kwa sababu ya kufuatilia kesi badala ya kufanya shughuli za maendeleo  na matokeo yake baada ya upande mmoja kushindwa unaanza kujenga  chuki na visasi hali inayoweza kuhatarisha amani na usalama. ’’amesema Jaji Mlacha.

Jaji huyo amezitaka Taasisi za Dini, vyombo vya Habari, Jeshi la Polisi pamoja na watendaji wa Mahakama kushirikiana katika kutoa Elimu na kuhamasisha umuhimu wa kutumia usuluhishi kama njia kuu ya kutatua na Kumaliza Migogoro pia Jamii imetakiwa kuwa tayari kujenga utamaduni wa kutafuta suluhu bila kufika kwenye vyombo vya Sheria.

‘‘Mtumie fursa ya nafasi mlizonazo katika kuhudumia Jamii kukutana na kuongea na wananchi juu ya umuhimu wa kutumia mbinu ya usuluhishi katika kutatua migogoro, kwani kwa kufanya hivyo mtajenga jamii yenye upendo, msamaha, ushirikiano na kuimarisha uchumi wa mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla’’ amesisitiza Jaji.

Aidha Jaji Mlacha amefafanua kuwa  Mwaka 2022 Mahakama zote mkoani Kigoma zilipokea na Mashauri 5366 ambapo yaliyoamuliwa kwa suluhu ni 256 sawa na Asilimia 4.8 na yaliyobaki yaliamuliwa na Mahakama kutokana na wahusika kukosa utayari wa kumaliza migogoro yao nje ya Mahakama.

Ameongeza kuwa, mkoa unachangamoto ya kukosa taasisi za nje ya Mfumo wa Mahakama zenye uwezo wa kuendesha vikao vya usuluhishi, baadhi ya Mahakimu kukosa  utayari wa kujitolea kufanya usuluhishi, ukosefu wa Elimu kwa jamii kuhusu umuhimu wa kumaliza migogoro bila kutegemea maamuzi ya kimahakama pamoja na tabia binafsi za baadhi ya wanajamii kutokubali kutoa msamaha kwa wanaowakosea.

‘‘Mahakimu mnawajibu wa kuwaelimisha wateja wenu kabla hawajaanza kusikiliza kesi zao kuhusu umuhimu wa kukaa na kusikilizana kisha kumaliza tofauti zao nje ya mahakama hususani kwa kesi zisizo za jinai, kwani hukumu za kimahakama zina machungu yake kwa upande wa anayehukumiwa’’ amesisitiza Mhe Jaji Mlacha.

Maadhimisho ya wiki na Siku ya Sheria Mwaka 2023 yameongozwa na Kauli mbiu isemayo ‘’UMUHIMU WA UTATUZI WA MIGOGORO KWA NJIA YA USULUHISHI KATIKA KUKUZA UCHUMI ENDELEVU: WAJIBU WA MAHAKAMA NA WADAU.


PICHA MBALIMBALI ZA HAFLA YA MAADHIMISHO YA WIKI NA SIKU YA SHERIA MKONI KIGOMA.


Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa