• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

WAHANDISI WAHIMIZWA KUSIMAMIA MIRADI KWA UKARIBU

Posted on: August 20th, 2023

UJENZI WA TANKI LA MAJI KATIKA KIJIJI CHA SONGAMBELE WILAYANI BUHIGWE KWA THAMANI YA SHILINGI MIL. 115 UMEZINDULIWA NA MBIO ZA MWENGE WA UHURU LEO AGOSTI 20,2023

MRADI WA UJENZI WA JENGO LA MAKAZI YA OFISI YA MKUU WA WILAYA YA BUHIGWE.KAIMU KATIBU TAWALA MIUNDOMBINU OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA FRANCISCO MAGOTI (KUSHOTO) AKITOA UFAFANUZI KUHUSU MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA JENGO LA MAKAZI YA MKUU WA WILAYA YA BUHIGWE KWA KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE ABDALLAH KAIM. WA KWANZA KULIA NI MKUU WA WILAYA YA BUHIGWE KANALI MICHAEL MASALA.VIJANA WAENDESHA BODABODA KASUMO WAKIMSIKILIZA KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE ADBALLAH KAIM (HAYUPO PICHANI) ALIPOTEMBELEA KIKUNDI HICHO NA KUKIZINDUA RASMIMUONEKANO WA SHAMBA LA MITI KATIKA MRADI WA HIFADHI YA MAZINGIRA, SHULE YA SEKONDARI KAHIMBA.KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE WA UHURU ABDALLAH KAIM AKIKAGUA KABLA YA KUWEKA JIWE LA MSINGI KATIKA ZAHANATI YA KIJIJI KASUMO WILAYANI BUHIGWE.

MRADI WA UJENZI WA MADARASA MANNE KATIKA SHULE YA SEKONDARI BUHA.

ABDALLAH KAIM AMBAYE NI KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE WA UHURU AKIZUNGUMZA NA WANAFUNZI(SHULE HAIKUFAHAMIKA) MARA BAADA YA KUPANDA MITI KATIKA MRADI WA UHIFADHI WA MAZINGIRA  KIJIJI CHA RUHEKA.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa 2023 Abdallah Kaim  amewaelekeza Wahandisi katika Halmashauri za Mkoa wa Kigoma kujenga tabia endelevu ya kufuatilia na kutembelea mara kwa mara miradi ya Maendeleo inayotekelezwa katika maeneo yao.

Kaim ametoa maelekezo hayo mara baada ya kukagua Mradi wa ujenzi wa madarasa manne katika Shule ya Sekondari Buha iliyopo wilayani Buhigwe na kusisitiza kuwa dosari ndogondogo zilizobainika katika mradi huo zimetokana na wahandisi kutokufuatilia kwa ukaribu zoezi la ujenzi wa baadhi ya miradi ya maendeleo katika maeneo wanayowajibika nayo.

‘’Hatutegemei kuona dosari ndogondogo zikiendelea kuonekana mara baada ya mradi kukamilika, hii ni ishara kuwa kuna baadhi ya wahandisi  hawatekelezi ipasavyo zoezi la kukagua hatua mbalimbali za utekelezaji wa baadhi ya miradi’’ Amesema Kaim.

Kiongozi huyo wa mbio za Mwenge kitaifa 2023, amesisitiza kuwa dosari zilizobainika wakati wa ukaguzi wa Miradi zifanyiwe kazi na taarifa ziwasilishwe kuendana na muda alioelekeza wa kufanyika kwa marekebisho hayo.

Aidha Kaim amewataka wananchi kuendelea kuchukua tahadhari pamoja na kujikinga na ugonjwa wa Marelia kwa kuzingatia matumizi sahihi ya vyandarua pamoja na kutumia dawa kwa ukamilifu pale wanapobainika kuwa na Maradhi hayo.

Upande wake Mratibu wa Marelia katika Halmashauri ya Buhigwe amesema Katika kipindi cha Mwaka 2022 hadi 2023 kitengo chake kimefanikiwa kutoa Elimu ya udhibiti wa marelia kwa walengwa 22,200.

Ameendelea kufafanua kuwa, changamoto ya matumizi sahihi ya vyandarua pamoja na kutozingatia usafi wa mazingira vimeendelea kusababisha kuwepo kwa ugonjwa huo katika Halmashauri  ya hiyo.

Aidha Mwenge wa Uhuru wilayani Buhigwe umetembelea mradi wa Hifadhi ya Mazingira katika Shule ya Msingi Kahimba, kuweka Jiwe la Msingi Zahanati ya kijiji Kasumo, Nyumba ya Makazi ya Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe pamoja na  Barabara ya Lami Buhigwe mjini.

Kadhalika Mwenge huo umezindua madarasa manne katika Shule ya Sekondari Buha, mradi wa pikipiki za kusafirisha abiria Kijiji cha Kasumo, ujenzi wa Tanki la Maji kijiji cha Songambele pamoja na kushiriki zoezi la kupanda miti katika kijiji cha Ruheka.

Miradi yote ikiwa na Thamani ya Shilingi Bil. 3.6 imepokelewa na Mwenge huo wa Uhuru

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa