• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

IDARA YA ELIMU WATAKIWA KUSHIRIKIANA NA WAZAZI ILI KUIMARISHA TAALUMA MKOANI KIGOMA

Posted on: December 12th, 2022

Idara ya Elimu Sekondari kwa kushirikiana na wazazi Mkoani hapa wametakiwa kuhakikisha wanafunzi wote waliofaulu Elimu ya Msingi wanajiunga na kuendelea na Masomo kwa ngazi ya Sekondari  katika Muhula Mpya wa Mwaka wa Masomo wa 2023.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mhe. Thobias Andengenye alipoanza Ziara yake ya kikazi wilayani Buhigwe ikiwa na lengo la kukagua  Maendeleo ya Ujenzi wa vyumba vya Madarasa ya Wanafunzi wanaotarajiwa kuanza Kidato cha Kwanza katika wilaya nane za Mkoa wa Kigoma.

Amesema wazazi kwa kushirikiana na wataalam wa Idara ya Elimu Sekondari wahakikishe wanaweka mikakati madhubuti yenye lengo la  kufanikisha wanafunzi wote waliofaulu Elimu ya Msingi na kuchaguliwa kujiunga na Elimu ya Sekondari,  wanafika na kuanza masomo  katika Shule  walizopangiwa ili waweze kupata haki hiyo ya kitaaluma.

‘‘Elimu ni haki ya Msingi kwa watoto wetu na ndio msingi wa ujenzi wa Taifa, hivyo hatua madhubuti zinatakiwa kuchukuliwa ili kujenga Taifa la watu wenye weledi kupitia upatikanaji na usimamizi mzuri wa kitaaluma  kwa watoto wetu’’ amesema.

Aidha amewaagiza wasimamizi na mafundi wanaotekeleza jukumu la ujenzi wa madarasa hayo, kuongeza kasi sambamba na kusimamia ubora wa kazi.

Naye Kaimu Afisa Elimu Mkoa wa Kigoma David Mwamalasi, amesema Mkoa wa ulipokea Jumla ya Shilingi 7, 160, 000,000 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba 328 vya Madarasa ya Kidato cha kwanza kwa Mwaka 2023 ambapo utekelezaji wa shughuli za ujenzi ulianza Oktoba 2022 kwa Halmashauri zote nane za Mkoa.

Ameendelea kufafanua kuwa, mpaka sasa ujenzi uko katika hatua mbalimbali ambapo vyumba sita vipo katika hatua ya ukuta, 21 hatua ya Lenta, 175 hatua ya upauaji, 156 hatua ya umaliziaji na hakuna shughuli inayoonyesha mkwamo kwa kuwa katika maeneo yote mafundi wapo kazini na wanaendelea vizuri na kazi.

Akiwa wilayani Buhigwe, Mkuu wa Mkoa amekagua maendeleo ya ujenzi wa Madarasa hayo kwa ajili ya Wanafunzi wanaotarajiwa kuanza kidato cha kwanza katika Shule za Sekondari Mnanila, Nyakimwe, Kibwigwa, Buyenzi, Muyama, Kahunga, Buha na Yanza.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • RC ANDENGENYE AKABIDHI VITENGO VITENGO VYA LISHE MKOA NA WILAYA UVINZA

    May 09, 2025
  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa