• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

GERARUMA ASISITIZA UTUNZAJI VYANZO VYA MAJI KIGOMA

Posted on: October 1st, 2022

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2022 Sahili Geraruma, ametoa Rai kwa wakazi wilayani Buhigwe  mkoani Kigoma kuendelea kutunza Mazingira kwa kupanda miti katika vyanzo vya Maji na pembezoni mwa Mto Malagarasi ili kuendelea kukitunza chanzo hicho kikuu cha Maji katika Ziwa Tanganyika.

Rai hiyo imetolewa leo Tarehe 1, Oktoba 2023 mara baada ya Kiongozi huyo wa Mbio za Mwenge kuzindua Mradi wa Kitalu cha Miti ya hifadhi ya Mazingira chenye Jumla ya Miche 1,031,000 unaotekelezwa na Taasisi isiyo ya kiserikali ya uhifadhi wa Mazingira, Bliss Green Generation katika kijiji cha Biharu kilichopo Kata ya Biharu wilayani Buhigwe mkoani hapa.

‘‘Maeneo mengi  vyanzo vya Maji vinazidi kukumbwa na tishio la kukauka, hivyo miti hii ipandwe katika maeneo hayo na hakikisheni mnailinda ili lengo mlilolikusudia liweze kutimia’’ alisisitiza Geraruma.

Aidha Kiongozi huyo wa Mbio za Mwenge, amewataka wananchi kuepuka kufanya shughuli za kibinaadam katika maeneo yote ya vyanzo vya maji huku akisisitiza kuzingatia sheria za Serikali zilizowekwa kwa ajili ya Ulinzi na utunzaji wa vyanzo hivyo.

Naye Lukindo Hiza ambaye ni Mkurugenzi wa Shirika la Uhifadhi wa Mazingira linalofadhili  Mradi huo kupitiaProgram ya Tuungane, amesema miche hiyo itagawiwa bure kwa wananchi wa maeneo hayo na yale ya jirani kwa lengo la uhifadhi wa bonde la mto Malagarasi.

‘‘Ifahamike kuwa, mto Malagarasi ndicho chanzo kikuu cha Ziwa Tanganyika, hivyo tusipotunza chanzo hicho tutapoteza urithi wetu wa asili ambao pia ni chanzo kimojawapo cha uchumi  kwa wakazi wa Mkoa wa Kigoma’’alisema Hiza.

Baadhi ya wananchi wa Kata ya Biharu, wameshukuru kuanzishwa kwa mradi huo kwa kueleza kuwa, miti hiyo itakapopandwa itaimarisha vyanzo vya maji, upatikanaji wa mvua  na kupendezesha mazingira.

‘‘Miti hii itarudishia miti ya awali iliyowahi kuwepo katika maeneo yetu, hivyo itakapokua na kustawi itarejesha tabia ya nchi kama iliyokuwepo awali kabla ya uharibifu mkubwa wa mazingira uliofanyika’’ alisema  Eliudi Mbiliti.

Uzinduzi wa Kitalu hicho cha Miti umefanyika baada ya kiongozi huyo wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kwa Mwaka 2022, kuzindua vyumba viwili vya madarasa Shule ya Sekondari Mnanila, mradi wa vijana (bodaboda) pamoja na kuweka jiwe la msingi Kituo cha Afya mwayaya ambapo miradi yote ina thamani ya zaidi ya Shilingi Milioni mia sita.

Aidha Mbio hizo za Mwenge wa Uhuru wilayani humo,  zimezindua Klabu ya wapinga Rushwa  katika shule ya Sekondari Munanila pamoja na Klabu ya kupinga matumizi ya dawa za kulevya katika Shule ya Msingi Milenda.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa