• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

DKT. MPANGO APIGA MARUFUKU WAZAZI KULIPIA KADI ZA KLINIKI

Posted on: July 12th, 2024

Makamu wa Rais wa Jymhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Mpango amemuagiza Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kupitia kwa Naibu wa Waziri wa Wizara hiyo Zainab Katimba kupitia upya Sheria Ndogo za  Sekta ya Afya katrika Halmashauri zinazoruhusu  kulipia kadi ya kliniki pamoja na kutoza faini kwa wanaojifungua nje ya vituo vya Afya ili kuzisitisha sheria hizo mara moja.

Makamu wa Rais ametoa agizo hilo Julai 12, 2024 akiwa katika ziara yake ya kikazi wilayani Kasulu ambapo amepokea malalamiko ya wanawake kutozwa faini kati ya Shilingi 40,000 hadi Shilingi 50,000 na kusisitiza kuwa kitendo hicho ni kinyume na sheria na utaratibu huo unapaswa kusitishwa.

‘‘Changamoto hii inaonekana kuwepo maeneo mengi ndani na nje ya mkoa wa Kigoma  hivyo ninaiagiza Wizara kupitia upya sheria hizo na kuandaa mwongozo wa kuziondoa kisha  mzishushe kwenye Halmashauri kwa ajili ya utekelezaji  ili kuhakikisha utaratibu huo haujirudii tena’’amesisitiza Dkt. Mpango.

Amesema ni jukumu la watendaji wa serikali kuielimisha jamii kuhusu umuhimu wa kujifungua katika vituo vya Afya na inapotokea mjamzito kajifungua nje ya kituo cha kutolea huduma za Afya wahudumu wanapaswa kumpokea na kumpatia huduma bila masherti yoyote.

Akitolea ufafanuzi na maelekezo kero mbalimbali za wananchi zilizowasilishwa kupitia ziara hiyo, Makamu wa Rais amemuelekeza Afisa Biashara wa mji wa Kasulukuepuka kutumia nguvu wakati wa ukusanyaji wa makusanyo ya Halmashauri sambamba na halmashauri zote kutekeleza agizo la Serikali la kutotoza ushuru wa mazao kwa mzigo usiozidi tani moja.

Aidha ameitaka Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kuongeza kasi katika kushughulikia utoaji wa vitambulisho vya NIDA ili kutoa Fursa kwa wananchi kuvitumia kuendana na matakwa ya Serikali.

Sambaba na hayo, Makamu wa Rais  ameuelekeza uongozi wa wilaya kupitia wakuu wa wilaya kuhakikisha wanatumia mbinu mbadala ili kuhakikisha ukosefu wa vitambulisho hivyo hauwanyimi fursa vijana kupata  kazi katika mashirika au taasisi binafsi ili waweze kujipatia kipato.

Katika hatua nyingineDkt. Mpango ameuelekeza Uongozi wa Mamlaka  ya Udhibiti wa Usafiri Ardhini (LATRA)kutekeleza jukumu lao la kutoa Elimu kwa Jamii badala ya kusumbua wamiliki wa vyombo vya Usafiri hususani waendesha pikipiki maarufu kama bodaboda

‘‘Jukumu lenu la Msingi ni kutoa elimu na kuhamasisha watumiaji wa barabara wanazingatia taratibu na miongozo na wale watakaobainika kushindwa kuzingatia taratibu hizo ndio wachukuliwe hatua na sio kushinda mnakamata vyombo hivyo kabla ya kutoa elimu kwa Umma’’ alisisitiza Dkt. Mpango.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa