• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

DKT. MPANGO AMPONGEZA RC ANDENGENYE KUIMARISHA UHUSIANO BAINA YA WATENDAJI WA SERIKALI NA CCM

Posted on: July 13th, 2024

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Mpango amesema mahusiano mazuri yaliyopo baina ya Uongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na uongozi wa Serikali ya Mkoa yamekuwa chachu ya kufikia malengo ya serikali kwenye utekelezaji wa miradi ya maendeleo mkoani Kigoma.

Mhe. Dkt. Mpango ametoa kauli hiyo alipokutana na viongozi wa CCM na kusisitiza kuwa, Mkuu wa Mkoa wa Kigoma amekuwa kiunganishi kizuri baina ya pande mbili hizo kutokana na kufanya kazi kwa uwazi na ushirikishaji.

Amesema kumekuwa na ushirikiano mkubwa baina ya wakuu wa wilaya, wakurugenzi wa mamlaka za serikali za mitaa pamoja na viongozi wa ngazi mbalimbali ndani ya CCM, jambo linalowapa fursa wananchi kupata taarifa sahihi kuhusu kazi zinazofanywa na kuendelea kuiamini serikali kupitia ushirikishwaji huo.

‘‘Nitoe pongezi zangu za dhati kwako Mkuu wa Mkoa kutokana na kushirikiana bega kwa bega na viongozi hao ambao ndio wawakilishi wa wananchi katika maeneo yao, jambo linalosababisha kuondoa migogoro na mivutano isiyo ya lazima katika usimamizi na utekelezaji wa kazi mbalimbali za miradi ya maendeleo mkoani hapa’’ amesema Makamu wa Rais.

Aidha Makamu wa Rais amewataka viongozi hao wa Chama Cha Mapinduzi kuwa wajumbe na mabalozi wazuri katika kuhamasisha wananchi kushiriki kwenye zoezi la uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura sambamba na kujitokeza kwenye mchakato wa uchaguzi wa serikali za mitaa kwa ajili ya kupiga au kupigiwa kura ili nchi iweze kupata viongozi bora.

Katika hatua nyingine Makamu wa Rais amepongeza uamuzi wa mkuu huyo wa mkoa kwa kwa kuruhusu wananchi wanaodaiwa kulima katika eneo la hifadhi ya Msitu wa Makere Kusini mwanzoni mwa Mwaka huu, kuwataka kuondoa mazao yao  bila kuzuiliwa na watendaji kutoka wakala wa Huduma za Misitu nchini(TFS).

‘‘Haiwezekani mtu analima mnamuacha, anapalilia mnamuangalia tu, wakati wa kuvuna ndipo mnaanza kupambana nae na kumnyang’anya mazao yake kwa kosa la kulima katika eneo la hifadhi, huo ni unyanyasaji mkubwa  kwa nini msiwadhibiti wakulima hawa katika hatua za awali ili wasilime kabisa bali mnakuja kuwasumbua wakati wa kuvuna? Hili linafikirisha sana’’ amesema Dkt. Mpango.

Pamoja na hayo, Makamu wa Rais amempongeza Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu kwa kuendelea kuelekeza fedha nyingi mkoani Kigoma kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa miundombinu kwa ajili ya kuboresha maisha ya wakazi mkoani Kigoma.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa