• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

DKT. MPANGO AHIMIZA JAMII KUTAMBUA UMUHIMU WA ELIMU

Posted on: July 6th, 2023

MAKAMU WA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA DKT. PHILIP MPANGO AKIWA KATIKA PICHA YA PAMOJA NA WANAFUNZI WA SHULE YA MSINGI MUYAMA  MARA BAADA YA KUSHUHUDIA  MAPOKEZI YA  MADARASA  MATATU NA  OFISI MBILI ZILIZOKARABATIWA NA BENKI YA TCB PAMOJA NA VIFAA VYA KITAALUMA IKIWEMO KOMPYUTA MOJA, MASHINE YA CHAPA PAMOJA NA MADAWATI 24. KUSHOTO KWAKE NI  MKUU WA MKOA WA KIGOMA  MHE. THOBIAS ANDENGENYE.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Mpango amehimiza Jamii kusimamia na kuipa kipaumbele Elimu ili kuboresha mifumo wa Maisha ya wakazi mkoani Kigoma.

Akizungumza kwa nyakati tofauti akiwa ziarani kwenye wilaya za Buhigwe na Kasulu mkoani hapa,  Dkt. Mpango ameitaka jamii mkoani kuhakikisha watoto wote wanasoma bila kujali hali zao za kiafya au jinsia na kuhitimu kulingana na kiwango watakachotakiwa kukifikia kuendana na miongozo ya kitaaluma.

Amesema Serikali inaendelea kuweka Mazingira bora na rafiki kwa ajili ya  ufundishaji na ujifunzaji, hivyo wazazi watumie fursa ya uwepo wa Miundombinu rafiki kwa utoaji na upatikanaji wa Taaluma, kuhakikisha watoto wanasoma na kufaulu ili waweze kujikomboa wao wenyewe na Taifa kwa ujumla.

Kiongozi huyo amewataka wazazi kutoruhusu wanafunzi  kuolewa au kushiriki vitendo visivyo vya kimaadili hali itakayochangia kushindwa kuendelea na Masomo hivyo kutofikia malengo tarajiwa.

‘’Wanafunzi jukumu lenu kubwa ni kusoma kwa bidii ili muweze kupata maarifa mapya, jambo litakalowasaidia kufaulu na kuwavusha hatua nyingine  katika Safari yenu ya Kitaaluma mpaka kufikia malengo mliyojiwekea’’ amesisitiza Mpango.

Pia Makamu wa Rais amewasisitiza walimu kuendelea kufundisha kwa bidii ili kuinua kiwango cha ufaulu mkoani Kigoma hali itakayoongeza idadi ya watalaam watakaolitumikia Taifa katika ngazi mbalimbali.

Katika kuongeza Motisha ya kitaaluma Shule ya Msingi Muyama  ambayo kiongozi huyo alisoma kwa ngazi ya Elimu Msingi, Dkt. Mpango ameahidi kutoa Fedha kiasi cha Shilingi Mil. 3 kila Mwaka kwa wanafunzi watakaofanya vizuri kitaaluma pamoja na Mwalimu kinara wa ufundishaji.

‘’Nakuelekeza Mkuu wa Wilaya ukae na wataalam  wa Idara ya Elimu Msingi ili muone namna bora ya kuanzisha Tuzo ambapo Mwanafunzi Bora Kitaaluma kati ya watakaohitimu Elimu ya Msingi  atapata Shilingi Mil. 1, Mwanafunzi  wa kike atakayefanya vizuri kitaaluma pia atapata Mil. 1 pamoja na Mwalimu ambaye somo lake wanafunzi watafanya vizuri’’ amesema Mpango.

Katika hatua nyingine Dkt. Mpango amewataka wakazi kujenga utamaduni wa kupanda miti rafiki kwa Mazingira ili kuhuisha vyanzo vya maji vilivyoathiriwa na uharibifu mkubwa wa Mazingira mkoani hapa.

Pia Makamu wa Rais amesisitiza upandaji wa miti ya matunda kwani mbali ya kutunza mazingira, itasaidia kuinua Uchumi wa wananchi kutokana na uuzaji wa matunda yatakayozalishwa.

Aidha Dkt. Mpango ametoa wito kwa wakazi, kujenga Mazingira rafiki kwa wawekezaji wenye Dhamira ya kuwekeza mkoani Kigoma ikiwemo kukodisha au kuwauzia ardhi kwa kufuata utaratibu utakaokuwa na tija kwa pande zote mbili.

‘’Niwaase ndugu zangu, siku zote  Maendeleo ya Mkoa wetu yataimarishwa na watu wenye nia ya kuwekeza na kutoa fursa za ajira kwa vijana wetu, hivyo mnatakiwa kutoa ushirikiano mkubwa kwa wenye nia kama hiyo wanapowafikia jambo litakaloimarisha kiuchumi na kuendelea kuufungua’’ amesisitiza Dkt. Mpango.

MKUU WA MKOA WA KIGOMA MHE. THOBIAS ANDENGENYE AKIZUNGUMZA NA WANAFUNZI PAMOJA NA WAKAZI WA  MUYAMA (HAWAPO PICHANI)



Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa