• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

DC KALLI AHIMIZA JAMII KUBADILIKA KIFIKRA ILI KUDUMISHA FAMILIA BORA

Posted on: May 15th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Salum Kalli ametoa wito kwa Jamii mkoani Kigoma kubadilika kutoka kwenye fikra na vitendo vyenye viashiria vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto na kuimarisha Maadili na Upendo katika Familia na Jamii kwa Ujumla.

Kalli ametoa wito huo alipomuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Kigoma kwenye Sherehe ya Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Familia ambapo kilele chake kimkoa kimefanyika katika viwanja vya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma.

Amesema Kauli Mbiu ya Maadhimisho hayo ya Amani Maadili na Upendo  kwa Familia Imara, inatukumbusha wazazi na walezi umuhimu wa kusimamia maadili mema na upendo miongoni mwa wanafamilia kwa lengo la kujenga jamii yenye amani, upendo na Mshikamano.

Kupitia hotuba yake, Kalli amesema Maendeleo makubwa ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano yanaendelea kuchangia kwa kiasi kikubwa kuporomoka kwa maadili katika Jamii kutokana na muingiliano mkubwa wa mila na desturi za kigeni katika mifumo ya kimaisha katika jamii.

‘’Matumizi ya mitandao ya kijamii, runinga pamoja na ufuasi mkubwa wa mitindo ya maisha ya kigeni, vimechangia kuhamasisha vitendo vya ngono, uhalifu wa kimitandao, msongo wa mawazo pamoja na kuingiza tamaduni zisizo na maadili mema kwa Taifa letu’’ amesema.

Ameendelea kusistiza kuwa, pamoja na Serikali kuchukua hatua mbalimbali kudhibiti vitendo vunjifu vya maadili na ukatili dhidi ya wanawake na watoto, bado kumekuwepo na matukio ya ukatili na unyanyasaji mkubwa dhidi ya kundi hilo.

‘’Kwa kipindi cha Januari hadi Disemba  2022,  jumla ya matukio ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto yalikuwa 12,163, huku sababu kubwa zikitajwa kuwa ni uwepo wa Imani potofu, mila na desturi zenye madhara kwa makundi hayo, umasikini unaosababisha wazazi kushindwa kutekeleza majukumu yao kifamilia pamoja na uelewa duni wa masuala ya haki na Sheria’’ amefafanua Kalli.

Aidha, Kalli amewasihi wanajamii kuzingatia Sheria za nchi, kudumisha Amani na Upendo,  huku akisistiza watendaji wa Serikali  kuendelea kutoa Elimu na msaada wa kisheria dhidi ya wahanga wa vitendo vya ukatili na unyanyasaji hususani wanawake na watoto.

Pia amewataka wataalam wa  Serikali kutoka sehemu na vitengo vya  Maendeleo na Ustawi wa Jamii, Elimu, Afya, Sheria na Dawati la Jinsia kuratibu na kutekeleza kwa ukamilifu Afua zote za kupambana na kudhibiti ukatili dhidi ya wanawake na watoto mkoani hapa.

Naye Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa wa Kigoma amesema Ofisi yake kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wanaosimamia haki za Wanawake na watoto katika Jamii wataendelea kujikita katika kutoa msaada wa kiushauri na namna ya kuvifikia vyombo vya Sheria ili kuhakikisha Jamii inaishi kwa haki, usawa na maelewano.

Mbwanji amesisitiza kuwa, iwapo watoto watapata malezi bora kutoka kwenye familia au jamii, itapunguza wimbi kubwa la mmomonyoko wa maadili na kukithiri kwa vitendo vilivyo kinyume na maadili katika jamii kwa siku za usoni.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa