• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

CHONGOLO ATOA SOMO UWEKEZAJI BANDARINI

Posted on: July 27th, 2023

Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Komredi Daniel Chongolo amewaasa Wananchi kuunga Mkono juhudi za Serikali katika  kushirikiana na wawekezaji kwa lengo la kuimarisha Uchumi wa Taifa.

Chongolo ametoa wito huo alipozungumza na wakazi pamoja na wanachama wa CCM Mkoa wa Kigoma na Katavi katika Uwanja wa Community Centre mjini Kigoma, akiwa katika ziara yake ya kutoa Elimu kuhusu Mkataba wa Ushirikiano wa Uwekezaji na Uendelezaji wa Bandari nchini.

Amesema Msimamo wa CCM ni kuweka Msukumo na kipaumbele katika kushirikiana na Sekta Binafsi hususani wawekezaji ili kuimarisha Uchumi kwa lengo la kuwaletea  Maendeleo Wananchi na Taifa kwa ujumla.

Ameendelea kufafanua kuwa, Serikali inatambua na haipo tayari kuingia Mkataba utakaolitia Hasara Taifa, bali dhamira ni kufanya maboresho makubwa katika uendeshaji wa Sekta hiyo ili iweze kuleta manufaa kiuchumi

‘’Mivutano mnayoendelea kuishuhudia na hoja zinazoendelea kujengwa na makundi mbalimbali kuhusu Mkataba huu zinatokana na vita ya kugombea fursa za kiuchumi dhidi ya mataifa ambayo tutaingia nayo ushindani wa kibiashara kupitia uwekezaji tunaoenda kuufanya’’ amefafanua.

‘’Niwahakikishie kuwa uwekezaji unaoenda kufanywa na Serikali sio tu utaimarisha Bandari ya Dar es Salaam tu bali hata zile zilizopo mikoani na kutoa fursa ya ajira pamoja na kuimarisha utoaji wa Huduma kwa Wateja kwenye Maeneo hayo’’ amesisitiza Chongolo.

Naye Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji Prof. Kitila Mkumbo (Mb) amesema Dhamira ya Serikali kwenye uwekezaji wa Bandari inalenga kuongeza uwezo wa kushughulikia mizigo ili iwahi kuwafikia walengwa na kutoa fursa ya kuhudumia Idadi kubwa ya wateja kwa muda mfupi, hali itakayosaidia kuongeza mapato ya ndani ya nchi.

Dkt. Mkumbo ameeleza ‘’Serikali ilifanya utafiti wa kina wenye lengo la kubaini Kampuni yenye uwezo mkubwa katika kutoa Huduma za Bandari kwa kuzingatia uzoefu, utendaji kazi mzuri pamoja na tija kwa Taifa hadi kufikia maamuzi ya kumpata  mwekezaji.

Amefafanua kuwa Lengo ni kuongeza uwezo katika kuzihudumia nchi zinazotumia Bandari ya Tanzania zikiwemo Zambia, Congo, Burundi, Rwanda na Uganda ili kutoruhusu uwezekano wa kupokea mizigo kupitia Bandari za nje hali itakayosababisha tupoteze fursa hiyo muhimu ya kujiimarisha kiuchumi.

 ‘’Rais wetu ni mpenda haki na ameruhusu Demokrasia hali inayotoa mwanya kwa watu kuchangia mawazo yao na hata kukosoa bali, mtambue lengo kuu la Serikali ni kutumia uwekezaji kama njia bora ya kuimarisha uchumi’’ amesisitiza Dkt. Kitila Mkumbo.

Naibu Waziri wa Uchukuzi  Atupele Mwakibete (Mb) amesema suala la uwekezaji bandarini ni la muda mrefu na maamuzi ya Serikali kubadilisha Mwekezaji yametokana na kuwepo kwa uendeshaji usio na Tija katika eneo hilo.

‘’Reli zetu zinauwezo wa kusafirisha mizigo hadi kufikia zaidi ya Tani Mil. 30 kwa Mwaka ambapo kwa sasa uwezo wetu ni tani Mil. 23, jambo linalolalamikiwa na wateja kutokana na mizigo mingi kushindwa kutoka kwa wakati bandarini na kuwasababishia hasara wafanyabiashara’’ amesisitiza Naibu Waziri Mwakibete.

Upande wake Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye amesema maboresho makubwa ya Miundombinu ya Uchukuzi na Usafirishaji mkoani Kigoma yatakuwa chachu katika kuongeza Ufanisi wa kibiashara mara baada ya uwekezaji huo muhimu katika Bandari kukamilika.

Amesema kwa kuwa mkoa unapakana na nchi jirani za Burundi na Congo uwekezaji huo utakapokamilika utatimiza dhamira ya Mhe. Rais Samia ya kuufanya mkoa wa Kigoma kuwa kitovu Biashara na Uchumi kwa ukanda wa Magharibi.



Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • RC ANDENGENYE AKABIDHI VITENGO VITENGO VYA LISHE MKOA NA WILAYA UVINZA

    May 09, 2025
  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa