• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

CCT KIGOMA YAMPONGEZA RC ANDENGENYE

Posted on: May 27th, 2024

MKUU WA MKOA WA KIGOMA KAMISHNA JENERALI MSTAAFU WA JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI MHE. THOBIAS ANDENGENYE AKIPOKEA TUZO YA KUTAMBUA UTENDAJI KAZI WAKE MZURI KUTOKA JUMUIA YA KIKRISTO TANZANIA (CCT) MKOA WA KIGOMA ILIYOKABIDHIWA NA BABA ASKOFU OSWARD BAVUMA AMBAYE NI MWENYEKITI WA JUMUIA HIYO MKOANI KIGOMA MEI 27,2024.

Jumuia ya Kikristo Tanzania (CCT) Mkoa wa Kigoma imekabidhi  Tuzo Maalum ya kutambua kazi nzuri inayofanywa na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma katika kuhahakisha wananchi wanapata Maendeleo pamoja na kusimamia amani, umoja na mshikamano kwa wakazi mkoani humo.

Akizungumza mara baada ya kupokea tuzo hiyo, Mkuu wa Mkoa, ameushukuru uongozi huo wa CCT na kuahidi kuendelea kushirikiana na viongozi wa madhehebu ya dini mkoani hapa kwa lengo la kuimarisha Amani na mshikamano kwani ndio msingi wa Maendeleo.

Amesema viongozi wa dini wananafasi kubwa ya kuzungumza na wananchi hivyo kupitia mahubiri yao wanapaswa kuendelea kuhamasisha na kuikumbusha jamii umuhimu wa kujenga familia zenye kuheshimu misingi ya Imani za kidini ili kuimarisha malezi yenye maadili kwa watoto.

Aidha Andengenye  ameitaka Jamii mkoani hapa kuendelea kujiimarisha katika Imani za kidini kwa lengo la kumtumikia Mungu na kuachana na Imani za kishirikina jambo linaloleta mifarakano na uvunjifu wa Amani.

Upande wake Mwenyekiti wa Jumuia ya Kikristo Tanzania (CCT) Mkoa wa Kigoma Askofu Osward Bavuma amesema zawadi iliyotolewa kwa mkuu wa mkoa ni salamu ya upendo kutoka kwa waumini walio chini ya umoja huo, ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Siku ya Jumuia ya kikristo Tanzania.

Kupitia salamu za jumuia hiyo, Askofu Bavuma amesema pamoja na mambo mengine, Jumuia hiyo inatekeleza kazi za utoaji wa huduma za kimalezi kwa vijana waliopo ngazi mbalimbali za kimasomo pamoja na kutoa misaada kwa watoto wanaoishi Mazingira hatarishi.

Sambamba na hayo, ameitaja changamoto ya uwepo wa Imani za kishirikina miongoni mwa wakazi hususani kuibuka  kwa wimbi la wapiga ramli chonganishi maarufu Kamchape kuwa ni janga la kiimani mkoani hapa.

Amesema, wananchi wanapaswa kubadilika na kuachana na Imani za kishirikina kwani zimekwisha sababisha athari kwa baadhi ya wakazi ikiwemo uharibifu wa mali, watu kujeruhiwa na baadhi ya wakazi kuyakimbia makazi yao.

Amesisitiza kuwa, uongozi wa CCT utaendelea kuunga mkono kazi nzuri zinazoendelea kutekelezwa na serikali ya awamu ya sita mkoani hapa kwa lengo la kuwaletea wananchi maendeleo endelevu kwa kutatua changamoto mbalimbali zilizokuwa zikiwakabili.

Makabidhiano hayo yaliyofanyika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, yameshuhudiwa na mkuu wa Wilaya ya Kigoma Salum Kalli aliyemuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Kigoma kwenye maadhimisho ya Siku ya Jumuia ya Kikristo kimkoa yaliyofanyika Mei 26, 2014 mkoani hapa.  


Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • RC ANDENGENYE AZINDUA RASMI ZOEZI LA UGAWAJI VYANDARUA KIMKOA

    May 27, 2025
  • JAMII INAPASWA KUZINGATIA CHANJO KUJILINDA NA MARADHI

    May 20, 2025
  • MRADI WA UHIFADHI MAZINGIRA WAZINDULIWA KIGOMA

    May 15, 2025
  • RC ANDENGENYE AKABIDHI VITENGO VITENGO VYA LISHE MKOA NA WILAYA UVINZA

    May 09, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa