• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

BINTI PROJECT KUENDELEA KUBORESHA HEDHI SALAMA VYUONI

Posted on: June 3rd, 2024

Mradi wa Binti (Binti Project) umetajwa kuwa mkombozi katika kuhakikisha watoto wa kike katika vyuo vya ufundi mkoani Kigoma wanatimiza ndoto zao kwa kuimarisha Afya ya Hedhi salama.

Akizungumza alipomuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Kigoma kwenye uzinduzi wa Mradi huo  sambamba na kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Hedhi Salama duniani, Dkt. Albert Mwesiga  amesema walezi na Jamii kwa ujumla wanapaswa kuwa chachu ya kuleta mabadiliko katika kuimarisha huduma za hedhi salama mkoani Kigoma.

Amesema mradi wa Binti unalenga kutoa elimu ya Afya kuhusu hedhi salama, uimarishwaji wa miundombinu kwenye vyuo  vya ufundi sambamba na ugawaji sodo kwa wananfunzi wa kike katika vyuo vya ufundi.

Aidha kupitia mradi huo, matarajio ni kuviwezesha vikundi vya akina mama wajasiriamali kupata mafunzo ya ushonaji wa taulo za kike sambamba na kuwapatia mashine za kushonea taulo hizo ambazo ni salama Zaidi kwa afya za watumiaji.

Aidha ametoa rai kwa wanufaika wote wa mradi huo wakiwemo wanafunzi wa vyuo vya ufundi na vikundi vya akina mama kuwa chachu ya kuleta mabadiliko katika kuimarisha huduma za hedhi salama kwenye Jamii.

Mkurugenzi wa Shirika lisilo la kiserikali la (AfriCraft) linaloratibu upatikanaji wa Sodo na utoaji wa Elimu kuhusu hedhi salama AfriCraft Kelvin Nicholaus amesema vyuo vya ufundi vimekuwa havipewi kipaombele katika utoaji elimu ya Hedhi salama jambo ambalo limelisukuma shirika hilo  kutoa elimu na huduma ya uboreshaji wa taulo za kike kwa wanachuo mkoani hapa.

Amesema kuwa mradi huo umezinduliwa mkoani kigoma na utaendelea katika mikoa mingine sita 6 iliyobakia ili kuwawezesha kupata taulo kwa matumizi zaidi ya mara Moja na kutoa elimu juu ya utengenezaji wa taulo hizi za kike kwa kipindi cha miaka miwili 2024/2026.

“Tumezingatia madhara anayoweza kupata mtoto wa kike na kutengeneza sodo hizi ambazo zitamuwezesha kuwa huru na kuweza kuyatimiza majukumu yake wakati anapokuwa kwenye hedhi bila kupata maambukizi ya magonjwa sambamba na kuaibika kwa kukosa sodo za kutumia wakati awapo hedhi” amesema Nicholaus.

Mradi huo ulianza mwaka 2020 na kwa sasa unatarajia kuwafikia zaidi ya wanafunzi wa kike 12,000 pamoja na Vyuo 15 vya ufundi katika mikoa  ya Tanga ,Kigoma, Dar es salaam, Morogoro, Rukwa, Lindi na Zanzibar.

Ameongeza kwa kusema kuwa shirika la Africraft linaendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na mashirika yasiyo ya kiserikali pamoja na ya serikali katika kuboresha suala la hedhi salama na upatikanaji wake kwa watoto wa kike.

Kwa upande wake Mwanachuo kutoka Chuo cha Kigoma Training College, Jackline Matias ameishukuru serikali kwa kushirikiana na wadau kwa kuligusa kundi hilo kwa sababu kwa kuwawezesha kupata taulo bure  na kuwaweka huru katika shuguli mbalimbali zikiwemo za kimichezo.

Maadhimisho hayo yameambatana na Kauli mbiu isemayo “Pamoja kwa Hedhi Rafiki Ulimwenguni “huku kauli mbiu ya Mradi ikiwa ni ‘’Uwezeshwaji wa msichana kupitia Hedhi salama”. 

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa