• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

BILIONI 5.78 ZAIDHINISHWA UBORESHAJI WA MIUNDOMBINU YA BARABARA

Posted on: November 14th, 2022

Zaidi ya Sh. 5.78 bilioni zimeidhinishwa kutumika katika ujenzi wa madaraja na ukarabati wa  Barabara chini ya wakala wa Barabara Mjini na vijijini (Tarura) Mkoani hapa.

Kiasi hicho cha Fedha kitatolewa mara baada ya Serikali kusaini Mikataba  18 na Makandarasi wanaotarajiwa kuanza kufanya utekelezaji wa kazi hizo katika Halmashauri nane za Mkoa wa Kigoma kwa mwaka wa Fedha 2022/2023.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma kabla ya utiaji saini  mikataba hiyo,  Kanali Michael Ngayalina ambaye pia ni Mkuu wa wilaya ya Buhigwe, aliwataka Makandarasi kutekeleza Miradi hiyo kwa kuzingatia muda wa mkataba pamoja na miongozo ya utendaji wa kazi inayotolewa na Serikali ili kufanya kazi zenye ubora na kuwaharakishia wananchi maendeleo.

‘’Barabara ni kiungo muhimu kwa Maendeleo ya wananchi kwani mbali ya kurahisisha mawasiliano, inarahisisha ukuaji wa uchumi wa Taifa kutokana na kuruhusu usafirishaji wa bidhaa mbalimbali za kibiashara’’ alisema.

 ‘’Serikali imewaamini nanyi mkatekeleze kazi hizo kwa uadilifu huku mkitanguliza uzalendo  badala ya kujali maslahi binafsi na kufanya kazi mlizopewa  kwa kiwango cha chini ili mpate faida kubwa.’’ alisistiza Kamali Ngayanila.

Kaimu Meneja wa TARURA Mkoa wa Kigoma, Senzia Maeda, alisema jumla ya kazi 20 za matengenezo ya barabara na ujenzi wa madaraja zilitangazwa  kwa mwaka wa fedha 2022/2023  kwa Halmashauri za Mji Kigoma-Ujiji na Kasulu pamoja na wilaya za Kigoma vijijini, Uvinza, Kasulu, Buhigwe, Kibondo na Kakonko ambapo kazi 19 zilipata makandarasi na moja kukosa kwa kutokidhi vigezo vya zabuni.

‘’ Mikataba iliyosainiwa kwa ajili ya utekelezaji wa kazi hizo  ina Thamani ya Shilingi 5, 784,699,286.00 na tunatarajia mara baada ya zoezi hili la kusaini mikataba, kazi zitaanza ndani ya muda mfupi ili kuwaondolea kero na adha ya usafiri wananchi katika maeneo yatakayoguswa na utekelezaji huo’’ alisema Maeda.

Naye Mkandarasi Dalali Abdallah, alisema anaishukuru Serikali kwa kuendelea kuwaamini Makandarasi wazawa katika utekelezaji miradi hiyo huku akiahidi kutekeleza kazi hiyo kwa uadilifu na uaminifu.

‘’Tutajitahidi kufanya kazi kwa kuzingatia muda na miongozo ya Serikali pia kuhakikisha kazi tunazofanya zinakuwa  kwenye kiwango bora kwa kuwa tunafanya kazi hizi kwa maslahi yetu tukiwa watanzani’’ alisema Dalili.

Kazi zitakazofanyika kupitia Zabuni hizo ni uboreshaji wa barabara kwa kiwango cha lami jumla ya Kilomita nane pamoja na kiwango cha Changalawe kwa zaidi ya Kilomita mia nne ikiwa ni barabara mbalimbali katika Halmashauri zote nane za Mkoa wa Kigoma.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa