• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

BIL 26 KUJENGA KAMOASI YA MUHAS KIGOMA MKATABA WASAINIWA

Posted on: November 25th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye amesema ujenzi wa Chuo Kikuu cha Afya  na Sayansi Shirikishi Muhimbili Kampasi ya Kigoma kutarahisisha upatikanaji wa Huduma bobezi za kiafya sambamba na kuongeza idadi ya watoa huduma za Afya mkoani Kigoma

Andengenye amesema hayo alipozungumza kwenye hafla ya utiaji saini Mkataba wa Ujenzi wa Majengo ya Chuo hicho Kampasi ya Kigoma na kusisitiza kuwa kukamilika kwa miundombinu hiyo kutatoa fursa kwa wataalam wa Afya mkoani Kigoma kupata mafunzo kwa vitendo na kuongeza ujuzi katika utoaji huduma za Afya.

Akiwasilisha taarifa ya hatua za utekelezaji wa mradi huo, Naibu Mratibu wa Mradi Dkt. Nathanael  Sirili amesema kazi hiyo inatekelezwa kupitia mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Uchumi  (HEET) kwa Thamani ya Shilingi 26,088,071,158.84 ukitarajiwa kukamilika ifikapo  Juni 2026 ambapo na kutekelezwa na Mkandarasi  China Jianxi International Co. Ltd.

Dkt. Sirili amesema mradi huo utahusisha ujenzi wa jengo la utawala, ukumbi wa mihadhara, maabara moja ya kompyuta, maabara sita za kufundishia na nyingine moja ya anatomia,  ukumbi mkubwa wa mikutano, bweni la wanafunzi, bwalo la chakula, uwanja wa kisasa wa mpira wa miguu pamoja na barabara za kuunganisha miundombinu  itakayojengwa.

Amesema Historia ya Chuo Kikuu cha Muhimbili inaanzia mwaka 1963 kama shule ya udaktari ambapo mpaka kufikia mwaka 2024 kinatoa programu za mafunzo mbalimbali ya kiafya zipatazo 101 kwa ngazi za Shahada, stashahada, uzamili na uzamivu.

Amesema ni dhamira ya Mhe, Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuimarisha mifumo ya utoaji wa Elimu ya Afya nchini ambapo kupitia Programu ya Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Uchumi (HEET)  Chuo kinatekeleza kazi za kuboresha miundombinu katika Kampasi ya Mloganzila na Kigoma.

Ameedelea kufafanua kuwa hadi kufikia Novemba 15, 2024, utekelezaji wa Mradi katika Kampasi ya Chuo hicho mkoani Kigoma ni pamoja na kupatikana kwa ardhi yenye ukubwa wa Hekta 19.1, kuandaa moango kazi wa matumizi ya eneo, kuandaa itifaki ya uanzishwaji wa eneo hilo sambamba na kuanza kwa usafi.

Amesema katika ujenzi utakaofanyika, jengo la utawala litakuwa na ofisi za watumiaji sitini, ukumbi wa mihadhara wenye uwezo wa kutumika na watumiaji 50, ukumbi mkubwa wa mikutani watumiaji 300, maabara sita za kufundishia zenye uwezo wa kuchukua wanafunzi sitini kila moja, maabara ya atomia yenye meza 29, bweni la wanafunzi 111, bwalo la chakula lenye uwezo wa kutumika na watumiaji 120 sambamba na ujenzi wa uwanja wa mpira wa miguu wa kisasa.

Aidha miundombinu hiyo itakapokamilika itakuwa na uwezo wa kupokea kwa hatua za awali jumla ya wanafunzi 300 kwa mwaka wa kwanza na kadri inavyoendelea itaweza kupokea jumla ya wanafunzi 5,673.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa