• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

ASILIMIA 77 YA WAZEE KIGOMA WAPATIWA VITAMBULISHO VYA MATIBABU

Posted on: October 3rd, 2023

NA GRADNESS KUSAGA-KIGOMA.

Serikali Mkoani Kigoma kupitia Idara ya Ustawi wa Jamii imefanikiwa kuwapatia Jumla ya wazee  42,202 sawa na Asilimia 77 vitambulisho vya matibabu huku wazee 3100 wakiunganishwa na Mfuko wa Bima ya Afya ya Jamii ulioboreshwa (iCHF) kwa lengo la kuwapunguzia usumbufu wakati wa matibabu.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Salum Kalli alipomuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Kigoma katika hafla ya Maadhimisho ya Siku ya Wazee Duniani ambayo kimkoa imefanyika katika Ukumbi wa Joy in The Harvest Manispaa ya Kigima/Ujiji

Amesema kuwa hadi sasa Hospitali 8 za Halmashauri za mkoa zimefanikiwa kuanzisha madirisha ya matibabu kwa wazee kwa lengo la kupunguza adha ya kusubiri upatikanaji wa matibabu kwa muda mrefu.

Aidha Mkuu huyo wa Wilaya amesema Mkoa wa Kigoma umeendelea kuunda mabaraza ya wazee katika ngazi zote kwa lengo la kurahisisha ukusanyaji wa changamoto mbalimbali zinazowakabili wazee hao ili kupata ufumbuzi wa pamoja na kuimarisha upatikanaji wa haki na Huduma sahihi‘’ amesema Kalli.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Dkt. Jesca Lebba  akimuwakilisha  Katibu Tawala Mkoa wa kigoma, amesema wazee ni hazina na tunu hivyo  jamii iendelee kuwatunza kwa kuwapatia kipaumbele katika mambo yote ili kuendelea kunufaika na ushauri pamoja na Maelekezo yao.

‘’Serikali mkoani Kigoma itaendelea kuhakikisha inatoa usaidizi kwa wazee ili waweze kuishi katika Mazingira Salama  na endelevu ambayo yatawapunguzia changamoto zitokanazo na mabadiliko yanayosababishwa na kukua kwa Teknolojia pamoja na  Maendeleo kwa ujumla’’ Amesema Lebba.

Naye katibu wa Baraza la wazee Mkoa Gideon Menyo ameishukuru Serikali kwa kufanya utafiti katika Hospitali binafsi pamoja na mashirika  mbalimbali yanayotoa huduma za Jamii ili kuhakikisha wazee wanapewa kipaumbele katika upatikanaji wa huduma mbalimbali  na kwa wakati.

  ‘’Tunafurahishwa na Huduma ya Mpishe Mzee kwanza’’ ambayo kupunguza athari ambazo zingejitokeza kwa wazee kutokana na kukosa huduma ikiwemo zile za matibabu kwa muda muafaka’’ Mzee Menyo

Maadhimisho ya siku ya wazee Duniani yamehudhuriwa na Katibu Tawala mkoa, Makatibu Tawala wasidizi Mkoa, Wakurugenzi wa Halmashauri za wilaya, Makamu Mwenyekiti wa Baraza la wazee Mkoa, Wataalamu kutoka mamlaka za serikali za mitaa, Wakuu na wawakilishi wa taasisi za serikali na taasisi zisizo za kiserikali za Help Age Tanzania, REDESO, IRC na EWAK, Viongozi wa Chama Cha Mapinduzi na madhehebu ya Dini.

Kauli mbiu ya Maadhimisho jayo kwa Mwaka 2023 yamebeba ujumbe usemao ‘’Uthabiti wa wazee kwenye Dunia Yenye Mabadiliko’’.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa