• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

ANDENGENYE AZINDUA MRADI WA UBORESHAJI USTAHIMILIVU WA TABIA YA NCHI

Posted on: June 6th, 2023

MKUU WA MKOA WA KIGOMA MHE. THOBIAS ANDENGENYE AKIPANDA MTI KUASHIRIA UZINDUZI WA MRADI WA UBORESHAJI WA USTAHIMILIVU WA TABIA YA NCHI MEI 6, 2023 KATIKA VIWANJA VYA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA.

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye amesema Serikali mkoani hapa inatambua athari hasi zitokanazo na mabadiliko ya hali ya hewa na iko tayari kuunga mkono juhudi zote zinazofanywa na wafadhili katika kukabiliana na kudhibiti hali hiyo.

Mkuu wa Mkoa ametoa kauli hiyo alipozungumza wakati wa Uzinduzi wa Mradi wa Uboreshaji Ustahilmilivu wa Tabia ya Nchi unaotarajiwa kuanza kutekelezwa katika wilaya zinazohifadhi wakimbizi mkoani Kigoma chini ya Mradi wa Pamoja wa Kigoma(Kigoma Joint Programme), Awamu ya Pili.

Amesema Uongozi wa Mkoa unafahamu Madhara yanayoletwa na mabadiliko ya hali ya Hewa na umeendelea kuchukua hatua mbalimbali ili kuikabili hali hiyo ikiwemo kutekeleza agizo la Serikali la upandaji wa Miti pamoja na kuhamasisha wananchi kupunguza matumizi ya Nishati ya kuni na Mkaa.

‘’Nafahamu mradi huu utatekelezwa kwa ushirikiano wa Mashirika ya kuhudumia wakimbizi pamoja na vitengo mbalimbali vilivyopo katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, nasisitiza mkatetekeleze kazi zenu kwa weledi na ubora ili kile kilicholengwa kiweze kufikiwa’’ amesisitiza.

‘’Huu ni mradi wa kwanza katika Awamu ya Pili ya Mradi wa Pamoja wa Kigoma, ambao umelenga kushirikisha Mashirika mbalimbali yanayohudumia wakimbizi kwa lengo la kusaidia kutatua changamoto mbalimbali kwa Jamii ambazo zinahifadhi wakimbizi katika baadhi ya Wilaya zetu mkoani hapa’’ Amesema Andengenye.

Upande wake Mwakilishi wa UNHCR nchini Tanzania Mahoua Parums amesema hadi sasa nchi ya Tanzania inaendelea kutoa Hifadhi na kuwahudumia zaidi ya wakimbizi 250,000 katika Kambi mbalimbali.

Tumefarijika na kuanzishwa kwa Mradi huu muhimu kwani jamii hizo zimekuwa mstari wa mbele katika kugawa walichonacho kwa lengo la kuwasaidia wakimbizi hivyo tunawashukuru na tunadhani kuna u muhimu wa kuwasaidia katika utunzaji wa Mazingira, kukabiliana na mabadiliko ya  Tabia ya nchi pamoja na upatikanaji wa Nishati.

Amesema inapotokea Jamii inapokea Idadi kubwa ya wakimbizi kwa kipindi cha zaidi ya Muongo Mmoja,  inakutana na changamoto kubwa zinazosababishwa na idadi kubwa ya watu ikiwemo uharibifu mkubwa wa Mazingira.

Uwepo wa wakimbizi mkoani Kigoma umeachangia kwa kiasi kikubwa katika kusababisha uharibifu mkubwa wa Mazingira kutokana na Ongezeko la Shughuli za kibinaadamu katika maeneo ya kambi pamoja na vijiji jirani na kambi hizo.

Naye Balozi wa Ufalme wa Ubelgiji nchini Tanzania Mhe. Peter Huyghebaert amesema Programu hiyo imeanzishwa mahususi ili kukabiliana na uharibifu mkubwa wa Mazingira uliofanyika katika  Maeneo yanayohifadhi wakimbizi mkoani Kigoma.

‘’Kipaumbele chetu katika kutekeleza mradi huu ni kuzigusa Jamii zinazohifadhi wakimbizi kwa muda mrefu kwani maeneo yameathrika kimazingira kwa kiasi kikubwa hivyo tunalazimika kuanzisha mpango huu ili kukabiliana na Athari zinazosababishwa na Mabadiliko ya Tabia ya nchi’’ amefafanua Balozi Huygerbaert.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa