• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

ANDENGENYE AWATAKA WAKAZI KIGOMA KUHESHIMU SHERIA ZA UTUNZAJI WA MAZINGIRA

Posted on: November 24th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Kamishna Mstaafu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mhe. Thobias Andengenye amewataka wakazi mkoani hapa kuzingatia Sheria kwa kutovamia na kufanya shughuli za kibinaadamu katika maeneo tengefu ya Hifadhi za Mazingira ili kuifanya dunia kuwa sehemu salama kwa vizazi vilivyopo na vijavyo.

Mkuu wa Mkoa ametoa kauli hiyo, alipokuwa akizungumza na wakazi wa kijiji cha Mpeta Wilayani Uvinza Mkoani hapa, mara baada ya uzinduzi wa zoezi la usimikaji nguzo na mabango kwa ajili ya kubainisha mipaka ya Hifadhi ya chanzo cha Maji cha Mto Malagarasi, linalotarajiwa kuanza kutekelezwa na Bodi ya Maji ya Bonde la Ziwa Tanganyika-Kigoma.

Amesema ongezeko la shughuli za kibinaadamu ikiwemo kilimo cha kuhama hama pamoja na ufugaji holela vimeendelea kusababisha athari kubwa za kimazingira, ambapo baadhi ya watu kwa makusudi wamekuwa wakiendesha shughuli hizo bila kujali mipaka inayowekwa na Serikali kwa lengo la kutunza mazingira.

‘‘Mbali ya kuwa ni chanzo kikuu kinachochangia Asilimia sabini ya Maji katika ziwa Tanganyika, Mto Malagarasi ni urithi wa Dunia kutokana na kuwa sehemu ya uhifadhi wa viumbe hai ambao wameanza kutoweka duniani kote, hivyo hatuna budi kuutunza’’ amesema Andengenye.

Mkurugenzi wa Bodi ya Maji Bonde la Ziwa Tanganyika Mkoa wa Kigoma Tamimu Mlimbo, amesema eneo linalotarajiwa kuwekewa mabango na usimikaji wa nguzo ili kuonyesha mipaka ya mto huo lina ukubwa wa Kilomita za mraba 42, likiwa limeathiriwa zaidi na shughuli za Kilimo na pamoja na ufugaji holela.

Amesema walishafanya vikao na wananchi wanaopakana na maeneo hayo kwa ajili ya kuwajengea uelewa kuhusu umuhimu wa zoezi hilo pamoja na hatua zitakazochukuliwa na Serikali iwapo ukiukwaji wa Sheria za uhifadhi wa vyanzo vya maji utajitokeza katika maeneo yatakayobainishwa.

‘‘Kwa sasa wananchi watatengewa maeneo maalum ya kupita ili kunywesha mifugo yao kwa lengo la kutoathiri shughuli za ufugaji, aidha tumejipanga kujenga mabirika ya kunyweshea mifugo ili kuyafanya maeneo ya hifadhi yabaki salama’’ amesema Mlimbo.

Mlimbo, amesisitiza kuwa maeneo owevu ni muhimu yahifadhiwe kwa sababu husaidia kuhifadhi maji yanapotokea mafuriko hivyo kupunguza  uwezekano wa maji hayo kufikia makazi ya watu na kusababisha maafa pamoja na uharibifu wa mali.

Naye shija Magota ambaye ni mkazi wa Kijiji cha Mpeta wilayani Uvinza,  amesema walishajengewa uelewa juu ya umuhimu wa zoezi hilo hivyo watatoa ushirikiano kwa kutofanya shughuli zozote za kilimo na ufugaji katika maeneo yatakayobainishwa kuwa ni hifadhi ya Mto Malagarasi.

Wakazi hapa walikuwa hawana uelewa wa kutosha kuhusu maeneo yasiyotakiwa kulisha mifugo na kulima mazao mbalimbali, hivyo kwa sasa tumepata uelewa na tutajielekeza katika maeneo yaliyoruhusiwa kiserikali kufanya shughuli zetu za uzalishaji mali. Amesema  Magota.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa