• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

ANDENGENYE ASISITIZA UTOAJI TAARIFA ZA MAENDELEO YA MIRADI YA SERIKALI

Posted on: November 23rd, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Kamishna Mstaafu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mhe. Thobias Andengenye amesema wananchi wanahitaji kupata taarifa za mara kwa mara na zenye uhakika kuhusu maendeleo ya miradi mbalimbali inayotekelezwa na Serikali mkoani Kigoma.

Mkuu wa Mkoa ametoa kauli hiyo alipokutana na Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa  Nishati Vijijini (REA) Mhandisi Hassan Saidy pamoja na Wabia wa Maendeleo katika Sekta ya Nishati wanaofadhili miradi ya kusambaza Nishati vijijini, walipomtembelea Ofisini kwake kwa Lengo la kujitambulisha pamoja na kuwasilisha Taarifa fupi ya hali ya Utekelezaji wa Miradi ya Umeme kwa Mkoa wa Kigoma.

‘‘Tunapotekeleza majukumu yetu ya kuwatumikia wananchi kuna kufikiwa au kutokufikiwa kwa Malengo, hivyo mnapotupatia taarifa za maendeleo ya kazi zenu inaturahisishia kuwapa wananchi taarifa sahihi na kuondoa tetesi au hali ya sintofahamu inayosababishwa na watu wasio na nia njema  wanaoshindwa kuheshimu kazi nzuri zinazoendelea kutekelezwa na Serikali’’ amesema Mhe. Andengenye.

Aidha Mkuu wa Mkoa amepongeza kazi nzuri ya usambazaji wa huduma hiyo muhimu mkoani hapa, huku akiwaasa wananchi watumie fursa ya uwepo wa umeme katika maeneo yao kwa lengo la kuboresha hali ya uzalishaji mali na kujiinua kiuchumi.

Akitoa taarifa ya hali ya uzalishaji wa Umeme Mkoani Kigoma, Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini,  Mhandisi Hassan Saidy, amesema Miradi ya Umeme iliyopo kwenye Mpango wa utekelezaji  kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023kimkoa ni pamoja na  Ujazilizi fungu 2B ambapo jumla ya vitongoji 210 vilivyopo katika wilaya za Uvinza, Kasulu, Kakonko, Kigoma vijijini na Buhigwe  vitanufaika.

Aidha ameitaja miradi mingine kuwa ni Mradi wa kupeleka Umeme kwenye vituo vya Afya  8 pamoja na pampu za Maji 17, mradi wa kupeleka Umeme sehemu za Migodi midogo, kilimo na aina zote za viwanda pamoja na maeneo yaliyo pembezoni mwa Mji na Majiji ambapo wilaya za Kigoma vijijini, Buhigwe, Kibondo, Kakonko, Uvinza na Kasulu zitanufaika.

‘‘Mpaka kufikia Novemba 2022, Jumla ya Vitongoji 883 kati ya 1,855 vya Mkoa wa Kigoma vimepelekewa Umeme huku vitongoji 972 ambavyo havijafikiwa na huduma hiyo hatua za uhakiki  wa taarifa na utekelezaji wake zinaendelea kufanyika ambapo pia utekelezaji utategemea upatikanaji wa Fedha’’ amesema Mhandisi Hassan.

Amesisitiza kuendendelea kushirikiana na wadau pamoja na uongozi wa mko katika kuhakikisha Miradi ya umeme vijijini inatekelezwa kwa mujibu wa mikataba inavyoelekeza ili kuharakisha upatikanaji wa huduma hiyo muhimu kwa Maendeleo ya wananchi.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa