• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

ANDENGENYE AHIMIZA VITA DHIDI YA UJINGA, MARADHI NA UMASIKINI ILI KUFIKIA MAENDELEO ENDELEVU

Posted on: December 9th, 2023

Jamii mkoani Kigoma imetakiwa kuendelea kushirikiana na Serikali katika juhudi zake za kukabiliana na maadui Ujinga, Maradhi na Umasikini ili kuufanya Mkoa na Taifa kwa ujumla kuweza kuwa na Uchumi imara na kujitegemea.

Kauli  hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye alipozungumza kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 62 ya Uhuru wa Tanzania Bara yaliyofanyika kimkoa katika Wilaya ya Kigoma, ambapo amesisitiza jamii kujenga tabia ya kufanya kazi kwa bidi ili kujiimarisha kiuchumi.

Amesema iwapo Jamii itafanikiwa kukabiliana na maadui hao watatu na kila mtu kutekeleza wajibu wake kwa ufasaha, kujituma pamoja na kudumisha amani na utulivu, uchumi wa mwananchi mmoja mmoja utazidi kuimarika na kulifanya  taifa kusonga mbele.

‘‘Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu anaendelea kuendesha mapambano dhidi ya maadui hao kwa kuboresha miundombinu mbalimbali inayoleta ufanisi katika utoaji wa huduma za jamii pamoja na kufungua fursa mbalimbali za kiuchumi’’ amesema Andengenye.

Andengenye amesema mkoa wa Kigoma unajivunia mapinduzi makubwa ya Miundombinu yanayoendelea kufanyika ikiwemo ukarabati wa Uwanja wa Ndege, Ujenzi wa Barabara mbalimbali kwa kiwango cha Lami, mkoa kuunganishwa na Umeme wa Gridi ya Taifa, uboreshwaji mkubwa wa miundombinu ya kujifunzia na kufundishia, ujenzi wa vyuo vikuu pamoja na ujenzi wa Hospitali ya Kanda ya Magharibi unaotarajiwa kuanza hivi karibuni.

Aidha katika kutekeleza shughuli mbalimbali zinazokwenda sambamba na maadhimisho hayo, Mkuu huyo wa Mkoa amegawa miche zaidi ya 2000 ya zao la chikichi kwa wakazi wa Kata ya Machinjioni kisha kuhitimisha maadhimisho hayo kwa kushiriki kufanya usafi katika soko la Nazareti katika  Manispaa ya Kigoma Ujiji.

Upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Salum Kalli amehimiza jamii wilayani humo kujenga Tabia ya kudumisha usafi ili kupunguza athari mbalimbali zinazoweza kusababishwa na maradhi na kupunguza nguvu kazi ya Taifa.

‘’Nashauri tabia hii ya kufanya usafi katika maeneo ya kutolea huduma za Umma na yale binafsi iwe endelevu,  tusisubiri mpaka tupewe shinikizo au kutokea matukio  bali tuifanye iwe tabia endelevu kwa usalama wa Afya zetu na wenzetu wanaotuzunguuka’’ amesema Kalli.

Maadhimisho hayo yametanguliwa na Mdahalo uliofanyika Desemba 8, 2023 uliolenga kuangazia mafanikio ya Miaka 62 ya Uhuru wa Tanzania Bara, uliofanyika katika Ukumbi wa Kigoma Social Hall Manispaa ya Kigoma Ujiji na kuongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa