• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

Uwekezaji

Mkoa wa Kigoma sasa umekuwa ni kivutio kikubwa cha wawekezaji wa aina mbalimbali. Hii inatokana na ukweli kwamba ni njia fupi ya kibiashara inayounganisha Bandari ya Kigoma na Eneo lote la Maziwa Mkuu na Bandari ya Dar es Salaam katika Bahari ya Hindi kupitia Reli ya Kati, Barabara ya Kati na Uwanja wa Ndege wa Kigoma. Mkoa ni mlango wa Biashara za kimataifa na imekuwa ni mvuto wa wawekezaji, imedhihirika kuwa Kigoma ni eneo zuri kimkakati kuendeleza Eneo Maalum la Uchumi kutoa huduma kwa nchi zinazolizunguka Ziwa Tanganyika.

Mkoa unaendesha mradi wa kuendeleza Eneo Maalum la Kiuchumi (Kigoma Special Economic Zone “KiSEZ”). Eneo la hekta 20,000 limeainishwa lakini kutokana na uwezo wa kifedha, Mkoa umepanga kutekeleza kwa awamu, ambapo awamu ya kwanza ina jumla ya hekta 691 na tayari shughuli mbalimbali zimefanyika ikiwa ni pamoja na:-

  • Upembuzi yakinifu (Feasibility Study)
  • Upimaji wa Eneo (Cadastral Survey)
  • Uthamini wa Mazingira (EIA)
  • Uthamini wa Mali (Valuation)
  • Mpango wa Matumizi ya Eneo (Master Plan)

Mpango wa kuendeleza Eneo Maalum la Kiuchumi Kigoma (KiSEZ) umefikia mahali ambapo ni muhimu kukamilisha malipo ya fidia na kuweka miundombinu ya nje, ili kuunga mkono juhudi za serikali ambazo zimekwishafanyika hadi sasa kuliendeleza eneo hilo.

Mkoa umeendelea kuchukua hatua za kuweka mazingira mazuri kwa wawekezaji na hivyo kupata wawekezaji makini wanne hadi sasa. Wawekezaji wawili wamejikita kwenye kilimo ambapo mwekezaji wa kwanza ni Kampuni ya Agrisol (T) Ltd. Kampuni hiyo iwepewa eneo katika Wilaya ya Kigoma eneo la Lugufu, ambapo watalima Maharage na Mahindi. Kampuni hii imeshafuata taratibu zote za uwekezaji kupitia Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC) na wanaanza kazi kwa kusafisha eneo la awamu ya kwanza lenye 500Ha wiki ijayo. Eneo hili watalima Mahindi 250Ha na Maharage ya Soya 250Ha; vile vile kampuni itajihusisha na usindikaji wa mazao yanayozalishwa katika shamba hilo. Mradi huu unataraijiwa kunufaisha wananchi katika ajira na kilimo cha mikataba (Outgrowers Scheme).

Kampuni ya pili inayowekeza kwenye kilimo inaitwa Kigoma Sugars Ltd. Ambapo itashughulikia kilimo cha Miwa katika Wilaya ya Kasulu, ambapo watajenga kiwanda cha sukari na kufua umeme wa mabaki ya miwa. Kampuni hiyo iko katika hatua za kukamilisha taratibu za uwekezaji kwenye kituo cha uwekezaji (TIC). Mradi huo utatekelezwa kwenye eneo la hekta 47,000 na unatarajiwa kuwa ni mradi mkubwa kuliko yote nchini, utakuwa unazalisha tani 6,000 kwa siku. Hivyo, mradi huo utaleta manufaa kwa wananchi katika ajira na kilimo cha mikataba (Outgrowers Scheme).

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • RC ANDENGENYE AKABIDHI VITENGO VITENGO VYA LISHE MKOA NA WILAYA UVINZA

    May 09, 2025
  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa