• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

BALOZI INDIA KUITANGAZA SEKTA YA UWEKEZAJI MKOANI KIGOMA

Posted on: March 9th, 2023

BALOZI WA INDIA NCHINI TANZANIA MHE. BINAYA PRADHAN AKIWA KATIKA PICHA YA PAMOJA NA MKUU WA MKOA WA KIGOMA KAMISHNA JENERALI MSTAAFU WA JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI MHE. THOBIAS ANDENGENYE, ALIPOMTEMBELEA OFISINI KWAKE MANISPAA YA KIGOMA/UJIJI.

Balozi wa India nchini Tanzania Mhe. Binaya Srikanta Pradhan amesema amedhamiria kuutangaza Mkoa wa Kigoma kiuwekezaji ili wafanyabiashara kutoka nchini mwake waweze kuzitambua Fursa na kufanya uwekezaji wenye Tija mkoani Kigoma.

Balozi Pradhan ametoa kauli hiyo aliposhiriki Mkutano wa Baraza  la Wafanyabiashara uliofanyika Mkoani hapa chini ya Chemba ya Wafanyabiashara, wenyeviwanda na Kilimo Tanzania(TCCIA).

Amesema amebaini uwepo wa fursa mbalimba za kiuwekezaji na zenye tija mkoani Kigoma na iwapo wawekezaji watatumia vizuri fursa hizo zitaweza kuwanufaisha wao binafsi pamoja, mkoa na nchi kwa ujumla.

Amefafanua kuwa, katika kuimarisha uhusiano mwema wa kibiashara na uwekezaji, Mpaka mwishoni mwa Mwaka 2022, nchi ya India ilifanikiwa kuwekeza zaidi ya Tril.10 katika shughuli mbalimbali za Biashara.

‘‘Serikali ya Awamu ya Sita imeendelea kufungua milango na  kutengeneza mazingira mazuri ya kiuwekezaj,i hali inayoendelea kusababisha ongezeko kubwa la wawekezaji kutoka nchini India kuja kuwekeza nchini Tanzania’’ amefafanua Balozi Pradhan.

Mbali ya uwekezaji kibiashara Balozi ameendelea kueleza kuwa, mahusiano ya nchi hizi mbili yaliyoasisiwa na Mwalimu Nyerere, yameendelea kuleta mazuri katika Sekta za Afya, Elimu, Madini, Maji na wananchi wa Nchi hizo kuishi  kwa kuheshimiana hususani kwa raia wa nchi hiyo wanaoishi Tanzania.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mhe. Thobias Andengenye amesema Mijadala na mazungumzo yanayofanyika baina ya wadau wa Maendeleo wa nchi hizi mbili katika kuangazia uwekezaji, italeta matokeo chanya  kwa pande zote mbili.

Amefafanua kuwa, Mkoa wa Kigoma una fursa nyingi za kiuwekezaji zikiwemo  zile za Kilimo cha Mazao ya Chakula na Biashara, Uwepo wa Eneo Maalum kwa ajili ya wawekezaji ''Kigoma Special Economic Zone''(KiSEZ), Biashara katika maeneo ya Mipaka zinazuhusisha nchi ya Tanzania na zile za Jirani, uwepo wa maeneo ya hifadhi za wanyama, uvuvi pamoja na Misitu.

Aidha Mkuu wa Mkoa amemsisitiza Balozi huyo na ujumbe wake  kuwa wajumbe wema na kwenda kuusemea vizuri mkoa wa Kigoma katika uhalisia wake hususani kufuatia kuwepo kwa maboresho makubwa ya miundombinu ya Usafiri na usafirishaji, Usalama, uimarishwaji mifumo ya wa Umeme, upatikanaji wa maji ya uhakika pamoja na mahusisano mema baina ya nchi ya Tanzania na zile za Jirani.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA August 05, 2019
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • BALOZI INDIA KUITANGAZA SEKTA YA UWEKEZAJI MKOANI KIGOMA

    March 09, 2023
  • LINDENI MIUNDOMBINU YA MAJI ILI TUWE NA MIRADI ENDELEVU-RC ANDENGENYE

    March 06, 2023
  • MAJALIWA AHITIMISHA ZIARA YAKE MKOANI KIGOMA

    February 27, 2023
  • MAJALIWA AHIMIZA KILIMO CHA MAZAO YA KIMKAKATI

    February 26, 2023
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255738192977

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa